Go to full page →

Kupinga Maelezo ya Watu Wengi TSHM 172

Kufuatana na namna watu wotewalivyo tafsiri ao kutambua Maandiko, Wolff akaandika: “Sehemu kubwa sana ya kanisa la Kikristo imepotoka kutoka kwa maana kamili ya Maandiko, na ... wanapofikiri kwamba wakati wanaposoma habari ya Wayahudi, wanapaswa kufahamu Mataifa,na wanaposoma Yerusalema, wanapaswa kufahamu kanisa; na kama inasemwa dunia, maana yake ni mbingu; na kwa kurudi kwa Bwana wanapaswa kufahamu maendeleo ya vyama vya wajumbe: na kupanda juu ya mlima wa nyumba ya Bwana, maana yake ni mkutano wa kundi kubwa la wamethodistes.” TSHM 172.3

Tangu miaka 1821 hata 1845, Wolff akasafiri katika Misri, Abisinia, Palestina, Syria, Persia, Bokhara, India, na Amerika. TSHM 172.4