Katika Ufunuo 14 malaika wa kwanza amefuatwa na wa pili, kutangaza, “Umeanguka, umeanguka, Babeli mji ule mkubwa, kwani umefanya mataifa yote kunywa mvinyo ya gazabu ya uasherati wake.” Ufunuo 14:8. Neno “Babeli” lilitoka kwa “Babel,” na maana yake ni machafuko. Katika Maandiko inaonyesha namna mbalimbali ya dini ya uongo ao ukufuru wa dini. Katika Ufunuo 17 Babeli inafananishwa kama mwanamke--mfano uliotumiwa katika Biblia kama mfano wa kanisa, mwanamke mwema hufananishwa na kanisa safi; mwanamke mwovu ni kama kanisa lililokufuru. TSHM 182.5
Katika Biblia ushirika kati ya Kristo na kanisa lake unafananishwa na ndoa. Bwana anasema: “Na nitakuoa kuwa wangu kwa milele, ndiyo, nitakuoa kwa haki.” “Mimi ni mme wenu.” Na Paulo anasema: “Niliwapatanisha ninyi kwa mme mmoja, ili niletee Kristo bikira safi.” Hosea 2:19; Yeremia 3:14; 2 Wakorinto 11:2. TSHM 183.1