Go to full page →

Ujumbe wa Malaika wa Pili TSHM 182

Katika Ufunuo 14 malaika wa kwanza amefuatwa na wa pili, kutangaza, “Umeanguka, umeanguka, Babeli mji ule mkubwa, kwani umefanya mataifa yote kunywa mvinyo ya gazabu ya uasherati wake.” Ufunuo 14:8. Neno “Babeli” lilitoka kwa “Babel,” na maana yake ni machafuko. Katika Maandiko inaonyesha namna mbalimbali ya dini ya uongo ao ukufuru wa dini. Katika Ufunuo 17 Babeli inafananishwa kama mwanamke--mfano uliotumiwa katika Biblia kama mfano wa kanisa, mwanamke mwema hufananishwa na kanisa safi; mwanamke mwovu ni kama kanisa lililokufuru. TSHM 182.5

Katika Biblia ushirika kati ya Kristo na kanisa lake unafananishwa na ndoa. Bwana anasema: “Na nitakuoa kuwa wangu kwa milele, ndiyo, nitakuoa kwa haki.” “Mimi ni mme wenu.” Na Paulo anasema: “Niliwapatanisha ninyi kwa mme mmoja, ili niletee Kristo bikira safi.” Hosea 2:19; Yeremia 3:14; 2 Wakorinto 11:2. TSHM 183.1