Go to full page →

Siri ya Mahali Patakatifu Inaelezwa TSHM 200

“Hema ya kweli” mbinguni ni Pahali patakatifu pa agano jipya. Wakati wa kifo cha Kristo, huduma ya kufananisha ilimalizika. Kwa sababu Danieli 8: 14 ilitimilika katika mgawo huu, Pahali patakatifu ambapo maneno haya yanaelekea ni Pahali patakatifu pa agano jipya. Hivyo, unabii, huu “Hata mangaribi na asubui ya siku elfu mbili mia tatu, halafu Pahali patakatifu patasafishwa” unaelekea Pahali patakatifu mbinguni. Lakini kusafishwa kwa pahali patakatifu maana yake ni nini? Mbinguni kunaweza kuwa kitu cha kusafishwa? Katika Waebrania 9 kusafishwa kwa Pahali patakatifu pa duniani na Pahali patakatifu pa mbinguni vinafundishwa wazi : TSHM 200.1

Karibu vitu vyote vinasafishwa kwa damu, na pasipo kumwanga damu hakuna ondoleo. Basi, mifano ya mambo yaliyo mbinguni ilipashwa kusafishwa hivyo [kwa damu ya wanyama] lakini vitu vya mbinguni yenyewe kwa zabihu nzuri zaidi kuliko hizi” (Waebrania 9:22,33), kwa damu ya zamani ya Kristo. TSHM 200.2