Go to full page →

Mukusudi ya Siri TSHM 233

Hapo kunakuwa pia ukumbusho wa zambi za watu. “Kwa maana Mungu ataleta kila kazi hukumuni, pamoja na kila neno la siri, kama likiwa jema ao kama likiwa baya.” Kila neno la bure watu watakalolisema. watatoa hesabu ya neno hili siku ya hukumu.” “Kwa masemo yako utahesabiwa haki, na kwa masemo yako utahukumiwa.” Makusudi ya siri yanaonekana katika kitabu, kwa maana Mungu “atatia nuru maneno yaliyofichwa katika giza, na kuonyesha makusudi ya mioyo.” Muhubiri 12:14; Matayo 12:36,37; 1 Wakorinto 4:5. Mbele ya kila jina katika vitabu vya mbinguni kunaingia kila neno baya, kila tendo la choyo, kila mapashwa yasiyotimizwa, na kila zambi ya siri. Maonyo yaliyotumwa na mbingu ao makaripio yasiyojaliwa, nyakati zilizotumiwa bure, mvuto uliotumiwa kwa wema ao kwa ubaya pamoja na matokeo ya mwisho wake wa mbali, yanaandikwa yote kwa taratibu na malaika mwandishi. TSHM 233.2