Go to full page →

Sura Ya 4 - Umoja na Kristo na Upendo wa Kindugu KN 49

(Mmoja na Kristo kwa Mungu)

MUNGU amekusudia kuwa watoto wake wapatane katika umoja. Je, hawatazamii kuishi pamoja katika mbingu moja? Je, Kristo amegawanyika? Je atawapa watu wake ushindi kabla ya watenda kazi, kwa nia moja, kutoa wakfu mioyo, akili na nguvu kwa kazi takatifu sana machoni pa Mungu? Umoja ni nguvu; utangano ni udhaifu. Tukiwa na umoja sisi kwa sisi, tukishirikiana kazini kwa moyo mmoja kwa ajili ya wokovu wa watu, tutakuwa kweli “wafanya kazi pamoja na Mungu.” Wale wanaokataa kufanya kazi kwa uelewano wanamwaibisha sana Mungu. Yule adui wa roho za watu hupendezwa kuona wakifanya kazi kwa kupishana. Watu kama hao huhitaji kukuza upendo wa kindugu na unyenyekevu wa moyo. Kama wangeweza kufungua pazia lisetirilo mambo ya wakati ujao na kuona matokeo ya baadaye ya kufarakana kwao hakika wangeona haja ya kutubu. 1[8T 240; KN 49.1