Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Ujumbe Uliotolewa na Watu Wanyenyekevu

    Kama wanafunzi wa elimu ya tabia na sifa za Mungu na dini walikuwa walinzi waaminifu, wenye bidii na wenye kuomba kuchunguza Maandiko, wangaliweza kujua wakati. Mambo ya unabii yangeweza kuwafungulia matokeo yaliyopashwa kuwa. Lakini ujumbe ulitolewa na watu wanyenyekevu. Wale waliozarau kutafuta nuru wakati inapokuwa karibu nao waliachwa gizani. Lakini Mwokozi anatangaza, “Yeye anayenifuata hatatembea katika giza, lakini atakuwa na nuru ya uzima.” Yoane 8:12. Kwa roho ile nyota fulani ya mwangaza wa mbinguni itatumwa kwake kwa kumwongoza katika ukweli wote.TSHM 147.1

    Kwa wakati wa kuja kwa mara ya kwanza kwa Kristo wakuhani na waandishi wa mji Mtakatifu wangaliweza kutambua “ishara za wakati” na kutangaza kuja kwa yule Aliyeahidiwa. Mika aliandika mahali pale pa kuzaliwa, Danieli, wakati wa kuja kwake. Mika 5:2; Danieli 9:25. Waongozi wa Wayahudi walikuwa bila sababu kama hawakujua. Ujinga wao ulikuwa matokeo ya zarau lenye zambi.TSHM 147.2

    Kwa faida kubwa sana waongozi wa Israeli wangalipashwa kujifunza pahali, wakati, hali ya mambo, ya tukio kubwa sana katika historia ya dunia--kuja kwa Mwana wa Mungu. Watu walipashwa kukesha ili wapate kumkaribisha Mkombozi wa ulimwengu. Lakini kule Betelehemu wasafiri wawili waliochoka kutoka Nazareti wakapitia njia nyembamba kwa mwisho wa upande wa mashariki ya mji, kutafuta kimbilio sababu ulikuwa usiku bila kuona mahali pa kupangia. Hakuna milango iliyofunguliwa kwa kuwapokea. Katika kibanda kibovu kilichotayarishwa kwa ajili ya mifugo, mwishowe wakapata kimbilio, na hapo Mwokozi wa ulimwengu akazaliwa.TSHM 147.3

    Malaika wakaagizwa kuchukua habari ya furaha kwa wale waliojitayarisha kuipokea na walioweza kwa furaha kuijulisha. Kristo alijishusha hata akajivika hali ya binadamu, kuchukua taabu isiyo na mwisho namna alipashwa kutoa roho yake sadaka kwa ajili ya zambi. Lakini malaika walitamani kwamba hata katika kujishusha kwake Mwana wa Aliyejuu angeweza kuonekana mbele ya watu na heshima na utukufu unaofaa tabia yake. Je, wakuu wa inchi hawangekusanyika kwa mji mkuu wa Israeli kusalimia kuja kwake? Je, malaika hawangemwonyesha kwa makutano yaliyomungojea?TSHM 147.4

    Malaika mmoja alizuru ulimwengu kuona wanani waliojitayarisha kumkaribisha Yesu. Lakini hakusikia sauti ya sifa kwamba mda wa kuja kwa Masiya umefika. Akakawia juu ya mji uliochaguliwa na hekalu ikasimama kwa mda mahali kuwako kwa Mungu kulionekana kwa miaka nyingi, lakini hata pale palikuwa na kutojali kwa namna moja. Wakuhani katika sherehe na kiburi walikuwa wakitoa kafara za unajisi. Mafarisayo kwa sauti kuu wakawaambia watu ao wakafanya maombi ya kujisifu kwa pembe za njia. Wafalme, watu wa elimu zote (philosophes), waalimu, wote walikuwa wasiokumbuka jambo la ajabu kwamba Mkombozi wa watu alikuwa karibu kuonekana.TSHM 148.1

    Kwa mshangao mjumbe wa mbinguni alikuwa karibu kurudi mbinguni pamoja na habari ya aibu sana, wakati alipovumbua kundi la wachungaji wakilinda makundi yao. Wakatamani sana kuja kwa Mkombozi wa ulimwengu. Hapa palikuwa na kundi la watu waliojitayarisha kumpokea mjumbe wa mbinguni. Kwa gafula utukufu wa mbinguni ukajaa pote katika uwanda, kundi lisilohesabika la wamalaika likafunuliwa; na kana kwamba furaha ilikuwa kubwa kwa ajili ya mjumbe kutoka mbinguni, wingi wa masauti kuimba wimbo wa furaha ambao mataifa yote ya waliookolewa wataimba siku moja: “Utukufu kwa Mungu aliye juu, na salama duniani, katika watu wanaomupendeza.” Luka 2:14.TSHM 148.2

    Fundisho la namna gani linakuwa kwa historia ya ajabu hii ya Betelehemu! Namna gani inakemea kutokuamini kwetu, kiburi chetu na hali ya kuwaza tunatosheka nafsini. Namna gani inatuonya kwa kujihazari, ili sisi vile vile tusishindwe kutambua ishara za nyakati na kwa hiyo hatutajua siku ya kuzuriwa kwetu.TSHM 148.3

    Si miongoni mwa wachungaji tu ambamo malaika walipata walinzi kwa ajili ya kuja kwa Masiya. Katika inchi ya wapagani vile vile kulikuwa wale waliomtazamia--watajiri, watu bora wenye akili— wenye elimu zote wa Mashariki. Kutoka kwa Maandiko ya Kiebrania walikuwa wakijifunza habari ya nyota kutokea kwa Yakobo. Kwa mapenzi ya bidii walingojea kuja kwake yeye aliyepashwa kuwa si “Faraja la Israeli” tu, bali “Nuru ya kuangazia Mataifa,” na “kuwa wokovu hata mwisho wa dunia.” Luka 2:25, 32; Matendo 13:47. Mbingu--ikatuma nyota ikaongoza wageni wa mataifa kwa mahali pa kuzaliwa kwa Mfalme mpya aliyezaliwa.TSHM 148.4

    Ni kwa “wale wanaomungojea” Kwamba Kristo “ataonekana mara ya pili, si tena kwa zambi, lakini kuokoa wale wanaomungojea kwa wokovu.” Waebrania 9:28. Kama habari ya kuzaliwa kwa Mwokozi, ujumbe wa kuja kwa mara ya pili haukutolewa kwa waongozi wa dini ya watu. Walikataa nuru kutoka mbinguni; kwa hiyo hawakuwa katika hesabu ya wale waliotajwa na mtume Paulo: “Lakini ninyi ndugu, si katika giza, hata siku ile iwapate ninyi kama mwizi: sababu ninyi wote ni wana wa nuru, na wana wa mchana: sisi hatuko wana wa usiku wala wa giza.” 1 Watesalonika 5:4, 5.TSHM 148.5

    Walinzi juu ya kuta za Sayuni walipashwa kuwa wa kwanza kupata habari ya kuja kwa Mwokozi, wa kwanza kutangaza ukaribu wa kuja kwake. Lakini walikuwa kwa raha, wakati watu walikuwa katika usingizi wa zambi zao. Yesu aliona kanisa lake, kama mti wa mtini usiozaa, umefunikwa na majani ya fahari, lakini pasipo kuwa na matunda ya damani. Roho ya unyenyekevu wa kweli, uvumilivu, na imani ilikosekana. Hapo kulikuwa kiburi, unafiki, uchoyo, ugandamizi. Kanisa laukufuru lilifunga macho yao kwa alama za nyakati. Wakatoka kwa Mungu na wakajitenga wao wenyewe kwa upendo wake. Namna walivyokataa na mapashwa yaliyowekwa, ahadi zake hazikutimizwa kwao.TSHM 149.1

    Wengi waliojidai kuwa wafuasi wa Kristo wakakataa kupokea nuru kutoka mbinguni. Kama Wayahudi wa zamani, hawakujua wakati wa kuzuriwa kwao. Bwana akapita pembeni yao na akafunua ukweli wake kwa wale ambao, kama wachungaji wa Betelehemu na Waakili wa Mashariki, walipewa usikizi kwa nuru yote walioyopokea.TSHM 149.2

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents