Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Siku Kuu ya Upatanisho

    Mara moja kwa mwaka, kwa Siku Kuu ya upatanisho, kuhani akaingia katika Pahali patakatifu pa patakatifu kwa ajili ya kutakaswa kwa Pahali patakatifu. Wana wawili wa mbuzi wakaletwa na kura ikapigwa, “kura moja ni ya Bwana na kura ingine ya Azazeli.” Walawi 16:8. Mbuzi wa Bwana akachinjwa kama sadaka ya zambi kwa ajili ya watu, na kuhani alipashwa kuleta damu ndani ya pazia na kuinyunyiza mbele ya kiti cha rehema na pia juu ya mazabahu ya uvumba mbele ya pazia.TSHM 201.2

    “Na Haruni ataweka mikono yake miwili juu ya kichwa cha yule mbuzi aliye hai, na kukiri juu yake maovu yote ya wana wa Israeli na makosa yao yote, hata zambi zao zote; naye ataziweka zote juu ya kichwa cha yule mbuzi aliye hai na kumutuma jangwani kwa mukono wa mutu aliye tayari, na yule mbuzi atachukua juu yake maovu yao yote mupaka inchi isiyo na watu; ataacha mbuzi kwenda zake jangwani.” Walawi 16:21,22. Mbuzi wa Azazeli hakurudi tena katika kambi la Israeli.TSHM 201.3

    Ibada ilikusudiwa kwa kuvuta Waisraeli kwa utakatifu wa Mungu na machukio yake ya zambi. Kila mutu aliombwa kuhuzunisha roho yake wakati kazi hii ya upatanisho ilipokuwa ikiendelea. Kazi zote zikawekwa kando, na Israeli alipashwa kutumia siku yenyewe katika maombi, kufunga, na kuchunguza moyo.TSHM 201.4

    Kiti kingine kilikubaliwa baadala ya mwenye zambi, lakini zambi hazikufutwa kwa damu ya kafara (mnyama); zilihamishwa kwa Pahali patakatifu. Kwa sadaka ya damu mwenye zambi akatambua mamlaka ya sheria, akatubu kosa lake, na akaonyesha imani yake katika Mukombozi atakaye kuja; lakini hakufunguliwa kabisa kwa hukumu ya sheria. Kwa Siku ya Upatanisho kuhani mkuu, anapokwisha kupata sadaka kwa makutano, akaenda ndani ya Pahali patakatifu pa patakatifu. Akanyunyiza damu ya sadaka juu ya kiti cha rehema, mara moja juu ya sheria, kufanya malipizi kwa madai yake. Halafu, kama mwombezi, akachukua zambi juu yake mwenyewe na kuzibeba kutoka kwa Pahali patakatifu. Kuweka mukono wake juu ya kichwa cha mbuzi wa Azazeli, yeye katika mufano akahamisha zambi hizi zote kutoka kwake mwenyewe hata kwa mbuzi. Ndipo mbuzi akazichukua mbali, na ziliangaliwa kwamba zilitengwa milele kutoka kwa watu.TSHM 201.5

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents