Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Sheria ya Uhuru

    Waalimu wengi wa dini wanatetea kwamba Kristo kwa mauti yake aliondoa sheria. Wengine wanaionyesha kama kongwa mzito wa kuhuzunisha, na kwa kinyume “utumwa” wa sheria walioonyesha “uhuru” wa kufurahia chini ya habari njema.TSHM 225.1

    Lakini si vile manabii na mitume walivyofanya mbele ya sheria takatifu ya Mungu. Akasema Dawidi: “Na nitatembea huru kwa kuwa nimetafuta maagizo yako.” Zaburi 119:45. Mtume Yakobo anatumia Amri kumi kama “sheria .kamili, ya uhuru.” Yakobo 1:25. Mfumbuzi anatangaza baraka juu yao “wanaoshika amri zake (wanaofua nguo zao), wawe na haki ya kula mti wa uzima, na kuingia katika mji kwa milango yake.” Ufunuo 22:14.TSHM 225.2

    Kama ingewezekana kwa sheria kugeuzwa ao kuwekwa pembeni, Kristo hangehitaji kufa kwa kuokoa mtu kwa azabu ya zambi. Mwana wa Mungu alikuja “kutukuza sheria na kuifanyiza kuwa na heshima.” Isaya 42:21. Akasema: “Musizanie nilikuja kuharibu torati”; “hata mbingu na inchi zitakapoondoka, yodi moja wala nukta moja haitaondoka, hata yote yatimie.” Juu yake mwenyewe akasema: “Ninafurahi kufanya mapenzi yako, Ee Mungu wangu; Ndiyo, sheria yako ni moyoni mwangu.” Matayo 5:17,18; Zaburi 40:8.TSHM 225.3

    Sheria ya Mungu haibadilike, ufunuo wa tabia ya Muumba wake. Mungu ni mapendo, na sheria yake ni mapendo. “Mapendo ni utimilifu wa sheria.” Asema mwandishi wa Zaburi: “Na sheria yako ni kweli”; “maana maagizo yako yote ni haki.” Paulo anasema: “Basi torati ni takatifu, na ile amri ni takatifu, na ya haki na njema.” Waroma 13:10; Zaburi 119:142,172; Waroma 7:12. Sheria kama hiyo inapaswa kuwa ya kuendelea kama Muumba wake. Ni kazi ya toba na utakaso kwa kupatanisha watu kwa Mungu kwa njia ya kuwapatanisha katika umoja pamoja na kanuni za sheria. Katika mwanzo, mutu alikuwa katika umoja kamili pamoja na sheria ya Mungu. Lakini zambi ikamtenga kwa Muumba wake. Moyo wake ulikuwa kwa vita juu ya sheria ya Mungu. “Kwa sababu nia ya mwili ni uadui juu ya Mungu, kwa maana haitii sheria ya Mungu, wala haiwezi.” Waroma 8:7. Lakini “Kwa maana Mungu alivyopenda ulimwengu, hata kutoa Mwana wake wa pekee,” ili mutu aweze kupatanishwa kwa Mungu, kurudishwa kwa umoja pamoja na Muumba wake. Badiliko hili ni kuzaliwa kupya, isipokuwa hivyo “hawezi kuona ufalme wa Mungu.” Yoane 3:16,3.TSHM 225.4

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents