Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    29 / SABABU GANI ZAMBI ILIRUHUSIWA?

    Wengi wanaona kazi ya uovu, na msiba wake na ukiwa, na wanauliza namna gani hii inaweza kuwa chini ya utawala wa Huyu Mmoja asiyekuwa na mwisho katika hekima, uwezo na upendo. Wale wanaotaka kuwa na mashaka wanashikamana na jambo hili na kutafuta sababu ya kukataa manene ya Maandiko matakatifu. Desturi ya asili na mafahamu mabaya ya maandiko yameficha mafundisho ya Biblia kuhusu tabia ya Mungu, asili ya mamlaka yake, na kanuni zake kuhusu zambi.TSHM 239.1

    Haiwezekani kueleza mwanzo wa zambi vilevile kama kutoa sababu kwa ajili ya kuwako kwake (zambi). Kwani kuna mambo mengi ya kutosha inayoweza kufahamiwa juu ya mwanzo na hali ya mwisho ya zambi kufanya onyesho kamili haki na wema wa Mungu. Mungu kwa hekima yo yote hakuwa mwenye madaraka kwa zambi; hapakuwa bila sababu kuondolewa kwa neema ya Mungu, hakuna upungufu katika mamlaka ya kimungu, iliyotoa nafasi kwa uasi. Zambi ni mpelelezi (mdukizi) ambaye kuwako kwake hakuna sababu inayoweza kutolewa. Kuisamehe ni kuitetea. Kama iliweza kusamehewa ingekoma kuwa zambi. Zambi ni onyesho la kanuni inayoleta kwa vita sheria ya upendo, inayokuwa msingi wa serkali ya Mungu.TSHM 239.2

    Mbele ya kuingia kwa zambi amani na furaha ilikuwa katika viumbe vyote. Upendo kwa Mungu ulikuwa mkubwa, upendo kwa mtu na kwa mwingine ulikuwa wa bila ubaguzi. Kristo Mwana wa pekee wa Mungu alikuwa mmoja pamoja na Baba wa milele katika hali, katika tabia, na katika kusudi--ni yeye peke yake ambaye aliweza kuingia katika mashauri yote na makusudi ya Mungu. ‘’Katika yeye vitu vyote viliumbwa vilivyo mbinguni, ... ikiwa ni viti vya wafalme ao usultani ao falme ao mamlaka.” Wakolosayi 1:16.TSHM 239.3

    Sheria ya upendo ilikuwa msingi wa utawala wa Mungu, furaha ya viumbe vyote vilivyoumbwa ilitegemea kwa upatano pamoja na kanuni zake za haki. Mungu hapendezwi na utii wa kulazimishwa, na kwa wote anatoa uhuru wa mapenzi, kwamba wanaweza kumfanyia kazi bila kulazimishwa).TSHM 239.4

    Lakini kulikuwa na mmoja aliyechagua kuharibu vibaya uhuru huo. Zambi ilianzia kwake, yeye aliyekuwa, baada ya Kristo, aliheshimiwa sana kwa Mungu. Mbele ya kuanguka kwake, Lusifero alikuwa wa kwanza kwa wakerubi wa kufunika, mtakatifu na mwenye usafi. “Bwana Mungu anasema hivi: Ulikuwa muhuri wa ukamilifu, mwenye kujaa na hekima na ukamilifu wa uzuri. Wewe ulikuwa katika Edeni, shamba la Mungu; kila jiwe la damani lilkuwa kifunuko chako. ... Wewe ulikuwa kerubi wa kufunika mwenye kutiwa mafuta; nami nilikuweka juu ya mlima mtakatifu wa Mungu; umetembea huko na huko katikati ya mawe ya moto. Ulikuwa mkamilifu kwa njia zako tangu siku ulipoumbwa, hata uovu ulipoonekana ndani yako. ... Moyo wako umenyanyuliwa kwa sababu ya uzuri wako, umeharibu hekima yako kwa sababu ya kungaa kwako.” “Nawe ulisema moyoni mwako ... Nitanyanyua kiti changu cha enzi juu kupita nyota za Mungu, Na nitakaa juu ya mlima wa makutano. ... Nitapanda juu kupita vimo vya mawingu, Nitafanana naaliye juu Sana.” Ezekieli 28:12-17; 28:6; Isaya 14:13,14.TSHM 239.5

    Kutamani heshima ambayo Baba aliweka juu ya Mwana wake, mtawala huyu wa malaika akatamani kwa uwezo ambao ulikuwa ni mamlaka ya Kristo peke yake kutawala. Sauti isiyopatana sasa ikaharibu mapatano ya mbinguni. Kujiinua kwa nafsi kukaamsha visirani vya uovu katika mioyo ambayo utukufu wa Mungu ulikuwa mkubwa. Baraza za mbinguni zikatetea pamoja na Lusifero. Mwana wa Mungu akaonyesha mbele yake wema na haki ya Muumba na tabia takatifu ya sheria yake. Kwa kuiacha, Lusifero angezarau Muumba wake na kujiletea uharibifu juu yake mwenyewe. Lakini onyo peke likaamsha msimamo. Lusifero akaruhusu wivu wa Kristo kushinda.TSHM 240.1

    Kiburi kikazidisha tamaa ya mamlaka. Heshima za juu zilizotolewa kwa Lusifero zikaleta kutokuwa na shukrani kwa Muumba. Akatamani kuwa sawa sawa na Mungu. Huku Mwana wa Mungu alikuwa Mfalme aliyekubaliwa wa mbingu, mmoja kwa uwezo na mamlaka pamoja na Baba. Katika mipango yote ya Mungu, Kristo alikuwa mshirika, lakini Lusifero hakuruhusiwa kuingia katika makusudi ya kimungu. “Sababu gani,” akauliza huyu malaika mkubwa, “inamupasa Kristo kuwa na mamlaka? Sababu gani yeye anaheshimiwa kupita Lusifero?”TSHM 240.2

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents