Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Wokovu wa Watu Wote Si Fundisho la Biblia

    Wanaoamini katika wokovu wa watu wote wanageuza Maandiko. Mhubiri anayejulikana wa Kristo anakariri uwongo ulioenezwa na nyoka katika Edeni, “Hakika hamutakufa.” “Siku mutakayokula matunda yake, macho yenu yatafunguliwa, na mutakuwa kama miungu. ” Anatangaza ya kama mwovu zaidi katika wenye zambi--muuaji, mwizi, mzinzi--baada ya kifo ataingia katika hali ya furaha ya milele. Hadizi za kweli za kupendeza, zinazofaa kwa kupendeza moyo wa tamaa za mwili!TSHM 262.5

    Kama ingekuwa kweli kwamba watu wote wangepita mara moja mbinguni kwa saa ya mwisho ya mauti, tungeweza vema kutamani mauti kuliko uzima. Wengi wameongozwa katika imani hii kumaliza wala kukomesha maisha yao. Kulemezwa na hatari na uchungu, inaonekana rahisi kuvunja mwendo wa maisha na kupanda upesi katika hali ya raha ya makao ya milele.TSHM 263.1

    Mungu ametoa katika Neno lake ushuhuda wazi ya kama ataazibu wavunjaji wa sheria yake. Je, yeye anakuwa mwenye rehema vilevile hata asitimize haki juu ya mwenye zambi? Tazama kwa msalaba wa Kalvari. Mauti ya Mwana wa Mungu inashuhudia kwamba “mushahara wa zambi ni mauti” (Waroma 6:23), kwamba kila uvunjaji wa sheria ya Mungu unapashwa kupata malipizi. Kristo asiyekuwa na zambi akawa mwenye zambi kwa ajili ya mtu. Akavumulia hatia za zambi na maficho ya uso wa Baba yake hata moyo wake ukapasuka na maisha yake kuangamizwa--yote haya ili wenye zambi waweze kukombolewa. Na kila nafsi ambayo inakataa kushirikiana na upatanisho uliotolewa kwa bei ya namna ile anapaswa kuchukua kwa nafsi yake mwenyewe hatia na azabu ya zambi.TSHM 263.2

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents