Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Kukosa Kiasi Kumetia Wengi Katika Mashaka

    Baraza za hukumu zimeharibika, watawala wamevutwa na tamaa kwa faida na upendo wa anasa za mambo ya uasherati. Kukosa kiasi kumetia wengi katika mashaka hivyo Shetani amekuwa na utawala karibu kamili juu yao. Wana sheria wamapotoshwa, wanavutwa kwa feza (rushwa), wamedanganyika. Ulevi na ulafi, udanganyifu wa kila namna, unaonekana miongoni mwa wale wanaosimamia sheria. Sasa Shetani hawezi tena kulinda ulimwengu chini ya utawala kwa njia ya kuzuia Maandiko, anatumia njia zingine kwa kutimiza kusudi lile lile moja. Kwa kuharibu imani katika Biblia ni kutumia pia kuharibu Biblia yenyewe.TSHM 285.3

    Ni kama katika miaka ya kwanza, alikuwa akitumika katika makanisa kuendelesha mashauri yake. Kwa kupinga mambo ya ukweli yasiyokuwa ya watu wengi katika Maandiko, wanatumia maelezo ambayo yanapenda kueneza mbegu za mashaka. Kushikama na kwa kosa la Papa la maisha ya milele ya asili na ufahamu wa mtu katika mauti, wanakataa ulinzi wa kipekee juu ya madanganyo ya elimu ya kuwa roho za watu waliokufa kurudi na kujionyesha na kuongea na watu (spiritualisme). Mafundisho wa maumivu mabaya ya milele yameongoza wengi kuwa kutoamini Biblia. Kwa madai ya amri ya ine yanavyoshurutisha, inaoonekana ya kuwa kushika Sabato ya siku ya saba kunaamriwa; na kwa namna inavyokuwa njia moja tu kwa kujiokoa wenyewe kwa shuguli ambayo hawataki kuifanya, waalimu wa watu wote wakatupilia mbali sheria ya Mungu na Sabato pamoja. Kama matengenezo ya Sabato inavyoenea, kukataa huku kwa sheria ya Mungu kwa kuepuka amri ya ine kutakuwa karibu kuenea pote. Waongozi wa dini wanafungua mlango kwa kumkana Mungu, kwa imani ya kuwa roho za watu waliokufa kurudi na kujionyesha na kuongea na watu (spiritualisme), na zarau kwa sheria takatifu ya Mungu-daraka la kutisha kwa uovu unaokuwako katika jamii la Kikristo.TSHM 286.1

    Kwani jamii lilelile linalodai ya kama mkazo wa kushika siku ya kwanza (dimanche) kungesitawisha mafundisho yahali ya kijamii. Ni mojawapo ya mashauri ya Shetani kuchanganya uwongo na ukweli shauri laonekana kuwa njema. Waongozi wa mwendo wa siku ya kwanza (dimanche) wangeshindania matengenezo ambayo watu wanahitaji, kanuni katika umoja pamoja na Biblia; lakini wakati ambao kunakuwa na madai pamoja na hizi kinyume kwa sheria za Mungu, watumishi wake hawawewzi kujiunga pamoja nao. Hakuna kitu kinachoweza kuthibitika kuweka kando amri za Mungu kwa ajili ya amri za watu.TSHM 286.2

    Katika makosa mawili makubwa, kutokufa kwa nafsi na utakatifu wa siku ya kwanza (dimanche), Shetani ataleta watu chini ya madanganyo yake. Wakati kosa la kwanza linapowekwa msingi wa imani ya kuwa roho za watu waliokufa hurudi na kujionyesha na kuongea na watu (spiritualisma), kosa la mwisho hufanya kifungo cha huruma pamoja na Roma. Waprotestanti wa Umoja wa Mataifa ya Kiamerika watakuwa wa kwanza kunyoosha mikono yao ngambo ya shimo kubwa kushika mkono wa imani ya kuwa roho za watu walikufa hurudi na kujionyesha na kuongea na watu (Spiritualisme); wakifikia kwa shimo kubwa kukumbatia mikono na mamlaka ya Roma. Na chini ya mvuto wa umoja huu wa mara tatu, inchi hii itafuata katika hatua za Roma kwa kukanyanga haki za zamiri.TSHM 286.3

    Kwa namna imani ya kuwa roho za watu waliokufa hurudi na kujionyesha na kuongea na watu (spiritualisme) , inakuwa na uwezo mkubwa kwa kudanganya. Shetani yeye mwenyewe “hujigeuza”. Ataonekana kama malaika wa nuru. Kwa njia ya imani ya kuwa roho za watu waliokufa hurudi na kujionyesha na kuongea na watu, miujiza itafanyika, wangonjwa wataponyeshwa, na maajabu mengi yasiyokukanishwa yatafanyika.TSHM 287.1

    Wafuasi wa kanisa la kiroma wanaojisifu juu ya miujiza kuwa alama ya kanisa la kweli watadanganyika upesi kwa uwezo huu wa kufanya miujiza; na Waprotestanti, wanapokwisha kutupia mbali ngao ya ukweli, watadanganyika vile vile. Wafuasi wa kanisa la Roma, Waprotestanti, na watu wapendao anasa za dunia wataonekana vivyo hivyo katika umoja huu mabadiliko makubwa kwa ajili ya toba ya ulimwengu.TSHM 287.2

    Kwa njia ya imani ya kuwa roho za watu waliokufa hurudi na kujionyesha na kuongea na watu (spiritualisme), Shetani hutokea kama mtenda mema wa kabila, kuponyesha magonjwa na kuonyesha kawaida mpya ya imani ya dini, lakini wakati ule ule anaongoza wengi kwa maangamizi. Kukosa kiasi kunaondoa akili; mapendeleo ya anasa, vita, na kumwanga damu hufuata. Vita huamsha tamaa mbaya sana ya nafsi na kufutia kwa milele mateka wake walioloanishwa katika uovu na damu. Nikusudi la Shetani kuchochea mataifa kwa vita, kwani anaweza kupotosha watu kwa matayarisho ya kusimama kwa siku ile ya Mungu.TSHM 287.3

    Shetani amejifunza siri za maumbile, na anatumia uwezo wake wote kutawala mwanzo kadiri Mungu anavyoruhusu. Ni Mungu anayelinda viumbe vyake kutoka kwa mharibu. Lakini jamii ya Ukristo limeonyesha zarau kwa sheria yake, na Bwana atafanya kile alichotangaza ya kwamba-angeondoa ukingaji wa ulinzi wake kwa wale wanaoasi kwa sheria yake na kukaza wengine kufanya pamoja. Shetani anakuwa na utawala wa wote ambao Mungu asio walinda kwa kipekee. Atasaidia na kusitawisha wengine, ili kuzidisha makusudi yake wenyewe; na ataleta taabu kwa wengine, na kuongoza watu kuamini ya kama ni Mungu ndiye anayewatesa.TSHM 287.4

    Anapotokea kama tabibu mkuu anayeweza kuponya magonjwa yao yote, Shetani ataleta ugonjwa na msiba hata miji ya watu waingie kwa maangamizi. Katika misiba baharini na inchini, katika mateketeo makubwa, katika tufani kali na mvua ya mawe, katika zoruba, garika, kimbunga, mawimbi ya maji kujaa, na tetemeko la inchi, katika namna maelfu, Shetani anatumia uwezo wake. Anaondolea mbali mavuno yenye kukomea yote, na njaa na taabu hufuata. Hugawanya mawaa ya mauti angani, na maelfu huangamia.TSHM 287.5

    Ndipo mdanganyifu mkubwa atashawishi watu kutwika taabu zao zote kwa wale wanaokuwa na utii kwa amri za Mungu ni laumu la daima kwa wakosaji. Itatangazwa ya kama watu wanamkosea Mungu juu ya mvunjo wa siku ya kwanza, ya kwamba zambi hii imeleta misiba ambayo haitakoma hata kushika kwa siku ya kwanza kutakapo kazwa kabisa. “Wale wanaoharibu heshima kwa ajili ya siku ya kwanza wanazuia kurudishwa kwa majaliwa ya Mungu na kufanyikiwa”. Kwa hivyo mashitaki yaliyofanywa ya zamani juu ya watumushi wa Mungu yatakaririwa. “Wakati Ahaba alipomuona Eliya, Ahaba akamwaambia: Ni wewe mwenye kutaabisha Israeli”? 1 Wafalme 18:17,18. Uwezo wa kufanya miujiza utatumia mvuto wake juu ya wale wanaomtii Mungu kuliko watu. “Pepo” watatangaza ya kama Mungu amewatuma kusadikisha wanaokataa siku ya kwanza kwa kosa lao. Watalilia uovu mkubwa ulimwenguni na kusaidia ushuhuda wa waalimu wa dini ya kama hali iliopoteza cheo cha mafundisho imaletwa na ukufuru wa siku ya kwanzaTSHM 288.1

    Chini ya utawala wa Roma, wale walioteseka kwa ajili ya habari njema walishitakiwa kama watenda maovu katika mapatano pamoja na Shetani. Ndivyo hivyo itakavyokuwa sasa. Shetani ataletea wale wanaoheshimu sheria ya Mungu kushitakiwa kuwa watu wanaoleta hukumu duniani. Kwa njia ya kutisha anajaribu kutawala zamiri, anasukuma watawala wa dini na wa dunia kukaza sheria za kibinadamu katika kuasi sheria ya Mungu.TSHM 288.2

    Wale wanaoheshimu Sabato ya Biblia watashitakiwa kuwa adui wa sheria na ukimya, kuvunja amri za maana za kijamii, kuleta machafuko ya mambo ya utawala na makosa, na kuita hukumu za Mungu inchini. Watashitakiwa juu ya chuki kwa serekali. Wajumbe wanaokana kanuni ya sheria ya Mungu wataonyesha kwa mimbara shuguli ya utii kwa utawala wa dunia. Katika vyumba vikubwa vya kufanya sheria na baraza za hukumu, wanaoshika amri watahukumiwa. Rangi ya uwongo itatolewa kwa maneno yao; maana mbaya kuliko itawekwa kwa mashitaki yao.TSHM 288.3

    Wakuu wa kanisa na serekali watajiiunga kwa kushawishi ao kushurutisha wote kuheshimu siku ya kwanza. Hata katika watawala wa Kiamerika wenye uhuru na wenye kufanya sheria watakubali matakwa ya watu wote kwa ajili ya sheria ya kukaza kushika siku ya kwanza. Uhuru wa zamiri ambao umegaramishwa kwa kafara kubwa hauta heshimiwa tena. Katika kuja kwa karibu kwa shindano tutaona kuonyesha kwa mfano maneno ya nabii, “Joka akakasirikia yule mwanamke, akakwenda zake kufanya vita juu ya wazao wake waliobaki, wanaoshika amri za Mungu, na kuwa na ushuhuda wa Yesu Kristo”. Ufunuo 12:17.TSHM 288.4

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents