Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Matokeo ya Zarau ya Maombi na Kujifunza Biblia

    Biblia haipashwi kujifunzwa pasipo maombi. Roho Mtakatifu peke yake anayetuwezesha kuona umuhimu wa vitu rahisi kufahamiwa, ao kutuzuia kupotoa mambo magumu ya kweli. Malaika wa mbinguni wanatayarisha moyo kufahamu Neno la Mungu. Tutapendezwa kwa uzuri wake, kugombezwa kwa maonyo yake na kutiwa nguvu na ahadi zake. Mara kwa mara majaribu huonekana kuwa na nguvu nyingi sana kwa sababu yule aliyejaribiwa hawezi mara hiyo kukumbuka ahadi za Mungu na kukutana na Shetani anayekuwa na silaha za Maandiko. Lakini malaika wanazunguka wale wanaotaka kufundishwa, na wataleta kwa ukumbusho wao ukweli unayohitajiwa.TSHM 292.6

    “Yeye atawafundisha ninyi vitu vyote, na kuwakumbusha ninyi vitu vyote niliyowaambia ninyi”. Yoane 14:26. Lakini mafundusho ya Kristo yanapashwa kwanza kuwekwa katika akili ili Roho ya Mungu ayalete katika ukumbusho wetu katika wakati wa hatari.TSHM 293.1

    Ajali ya makutano mengi sana inakuwa karibu kukusudiwa. Kila mshiriki wa Kristo inampasa kudai kwa bidii: “Bwana unataka nifanye nini”? Matendo 9:6. Inatupasa sasa kutafuta maarifa ya ndani na ya nguvu katika vitu vya Mungu. Hatuna na wakati kwa kupoteza. Tunakuwa kwa udongo wa kupendeza wa Shetani. Zamu wa Mungu usilale!TSHM 293.2

    Wengi hushangilia wao wenyewe kwa matendo mabaya ambayo wasiyoyafanya. Haitoshi ya kama wao ni miti katika bustani ya Mungu. Inawapasa kuzaa matunda. Katika vitabu vya mbinguni wanaandikwa kama walimaji wa udongo. Kwani kwa wale waliozarau rehema ya Mungu na wakatumia vibaya neema yake, moyo na upendo wa uvumilivu ungali ukitetea.TSHM 293.3

    Wakati wa mvua hakuna tofauti ya kuonekana kati ya miti na miti ingine; lakini wakati wa kipwa na upepo na majira ya baridi inapofika, miti isiyokauka inadumu imara wakati miti ingine inapo ponoa majani yao. Acha upinzani uamke, acha kutovumilia kutikisika tena, acha mateso iwashwe, na mapenzi yasiyo na bidii na ya unafiki ikubali imani; lakini Mkristo wa kweli atasimama imara, imani yake kuzidi kuwa hodari; tumaini lake kuzidi kungaa, kuliko siku za mafani-kio.TSHM 293.4

    “Maana atakuwa kama mti uliopandwa kando ya maji, unaofikisha mizizi yake karibu ya mto; hautaona woga wakati wa jua kali linapokuja, lakini majani yake yatakuwa mabichi; wala hautahangaika mwaka wa uchache wa mvua, wala hautaacha kuzaa matunda”, Yeremia 17:8.TSHM 293.5

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents