Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Machafuko Yanakaribia

    Kwa namna machafuko yanavyokaribia, jamii kubwa ya walioungama imani katika ujumbe wa malaika wa tatu, lakini hawakutakasiwa kwa njia ya utii kwa ukweli, wataacha nia yao na kujiunga kwa upinzani. Kwa kujiunga pamoja na ulimwengu wamefikia kuona mambo karibu ya nuru ya namna moja, na wanachagua upande wa watu wengi. Watu ambao kwanza walifurahi katika ukweli wanatumia kipawa chao na hadizi za kupendeza kwa kuongoza vibaya roho. Wanakuwa adui wakali wa ndugu zao wa kwanza. Waasi hawa ni wajumbe wa nguvu wa shetani kwa kueleza vibaya na kushitaki wanaoshika Sabato na kuchochea watawala kwa kuwapinga.TSHM 296.3

    Watumishi wa Bwana wametoa onyo. Roho ya Mungu imewalazimisha. Hawakushauriana na faida zao za mda, wala hawakutafuta kulinda sifa yao ao maisha yao. Kazi inaonekana kuwa mbali kabisa na uwezo wao kuitimiza. Kwani hawawezi kurudi nyuma. Kuona uzaifu wao, wanakimbilia kwa Mwenye Uwezo kwa kutaka nguvu.TSHM 297.1

    Nyakati mbalimbali katika historia zimeonyeshwa na maendeleo ya ukweli wa kipekee, uliofanyizwa kwa mahitaji ya watu wa Mungu kwa wakati ule. Kila ukweli mpya umefanya namna yake juu ya upinzani. Mabalozi wa Kristo wanapashwa kufanya wajibu wao na kuacha matokeo kwa Mungu.TSHM 297.2

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents