Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Upinzani Umeongezeka kwa Kimo Kipya

    Jinsi ushindani umeongezeka kwa nguvu nyingi; watumishi wa Mungu wanahangaika tena, kwani inaonekana kwao ya kama wameleta taabu. Lakini zamiri na Neno la Mungu vinawahakikishia ya kama mwenendo wao ni wa haki. Imani yao na uhodari umeongezeka pamoja na ujushi. Ushuhuda wao ni “Kristo ameshinda nguvu za dunia, je, tutaogopa ulimwengu uliokwisha kushindwa”?TSHM 297.3

    Hakuna mtu anayeweza kutumikia Mungu pasipo kujiweka kwa kosa yeye mwenyewe kinyume cha ushindani wa majeshi ya giza. Malaika waovu watamshambulia, kukilisha hatari ya kuwa mvuto wake unapata mawindo kutoka mikononi mwao. Waovu watatafuta kumtenga kwa Mungu kwa njia ya majaribu ya kutamanisha. Wakati haya hayafaulu, uwezo hutumiwa kwa kushurutisha zamiri.TSHM 297.4

    Lakini kwa namna Yesu anavyodumu kuwa Muombezi wa mtu katika pahali patakatufu juu, mvuto unaozuia wa Roho Mtakatifu huonekana kwa watawala na watu. Wakati watawala wetu wengi wanapokuwa wajumbe wa nguvu wa Shetani, Mungu vivyo hivyo anakuwa na wajumbe wake miongoni mwa watu wanaongoja katika taifa. Watu wachache watadumu kwa kuzuia maendeleo ya nguvu ya uovu. Ushindaji wa adui wa ukweli utazuiwa ili ujumbe wa malaika wa tatu uweze kufanya kazi yake. Onyo la mwisho litasimamisha uangalifu wa watu hawa waongozi, na wengine watalikubali nakusimama pamoja na watu wa Mungu kwa wakati wa taabu.TSHM 297.5

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents