Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Katika Mji Mtakatifu

    Po pote kwa jeshi lisilohesabika la waliokombolewa kila jicho limekazwa kwa Yesu. Kila jicho linatazama utukufu wake ambaye “uso wake ulikuwa umeharibiwa sana zaidi ya mtu ye yote, na sura yake zaidi ya watoto wa watu”. Isaya 52:14. Juu ya vichwa vya washindaji Yesu anaweka taji ya utukufu. Kwani kila mmoja kule kunataji ambalo lina “jina jipya” lake mwenyewe (Ufunuo 2:17) na mwandiko “Utakatifu kwa Bwana”. Katika kila mkono kumewekwa tawi la ngazi la ushindi na kinubi chenye kungaa. Ndipo, wakati malaika wenye kuamrisha wanapopiga sauti, kila mkono unapiga juu ya nyuzi na mguso wa ufundi mzuri sana, mkazo wa masauti. Kila sauti inainuliwa kwa sifa za shukrani: “Kwa yeye aliyetupenda na kutuosha zambi zetu kwa damu yake, na kutufanya kuwa wafalme wa makuhani kwa Mungu na Baba yake; kwa yeye ni utukufu na uwezo hata milele na milele”. Ufunuo 1:5,6.TSHM 313.5

    Mbele ya makutano ya waliokombolewa ni Mji Mtakatifu. Yesu anafungua milango, na mataifa yaliyolinda ukweli wanaingia ndani. Ndipo sauti yake imesikiwa, “Kujeni, ninyi muliobarikiwa na Baba yangu, mriti ufalme muliotengenezewa tangu kuumbwa kwa ulimwengu”. Matayo 25:34. Kristo anaonyesha kwa Baba yake ununuzi wa damu yake, kusema; ‘’Tazama, mimi ni hapa pamoja na watoto ulionipa “Wale ulionipa niliwachunga”. Waebrania 2:13; Yoane 17:12. Ee, furaha ya saa ile wakati Baba wa milele, kutazama kwa waliokombolewa, watatazama mfano wake, uharibifu wa zambi ukisha ondolewa, na binadamu mara ingine tena katika umoja na Mungu!TSHM 314.1

    Furaha ya Mwokozi ni kwa kuona, katika ufalme wa utukufu, mioyo iliyookolewa kwa maumivu yake makali na unyenyekevu. Mtu aliyeokolewa atashiriki katika furaha yake; wanatazama wale waliopatikana kwa njia ya maombi yao, kazi, na kafara ya upendo. Shangwe itajaa katika mioyo yao wakati wanapoona yule aliyeokoa wengine, na hawa zaidi na wengine.TSHM 314.2

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents