Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Uhodari wa Kutukana Mungu

    Mmojawapo wa “mapadri” wa agizo jipya akasema: “Mungu, kama Unakuwako, lipisha kisasi cha matukano yanayofanywa kwa kutukana jina iako. Ninakualika! Unakaa kimya; Husubutu kutuma ngurumo zako. Nani baada ya hii atakayeamini kuwako kwako tena?” Ni jibu gani hili la swali la Farao: “Bwana ni nani, nisikie sauti yake?”TSHM 128.6

    “Mupumbafu amesema moyoni mwake: Hakuna Mungu.” Na Bwana anasema, “Upumbafu wao utaonyeshwa wazi kwa watu wote.” Zaburi 14:1; 2 Timoteo 3:9. Wakati Ufransa ulipokataa ibada ya Mungu mwenye uhai haukukawia kushuka katika ibada ya haya ya kuabudu Mungu wa kike wa Akili (kutumia akili), mwanamke msharati. Ibada hii ikaanzishwa kwa msaada wa mkutano wa taifa! Mojawapo wa sherehe ya wakati huu wa wazimu kusimama inayopita yote kwani upumbafu ilichanganyika na ukosefu wa heshima kwa Mungu. Milango ya mapatano ikafunguliwa wazi wazi. ... Washiriki wa utawala wa mji wakaingia katika mwandamano wa taratibu, kuimba wimbo kwa sifa za uhuru, na kufuatana, kama kitu cha ibada ya wakati ujao, mwanamke mmoja aliyefunikwa, waliyemwita Mungu wa Kike wa Kutumia Akili. Alipokuwa katika baraza ya hukumu, wakamvua mwili wote kwa heshima, na wakamweka upande wa kuume wa msimamizi, ambapo alipojulikana kwa kawaida kama binti mchezaji wa mchezo wa kuigiza (opera).TSHM 129.1

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents