Go to full page →

Bwana Anahamakia Shetani TSHM 235

Na kwa mushitaki anasema: “Bwana akuhamakie, Ee Shetani. Ndiyo Bwana aliyechagua Yerusalema, akuhamakie. Hiki si kinga kilichoondoshwa katika moto?” Zekaria 3:2. Kristo atavika waaminifu wake kwa haki yake mwenyewe, ili aweze kuwaonyesha kwa Baba yake “kanisa la utukufu, pasipo alama wala kikunjo wala kitu cho chote kama hivi.” Waefeso 5:27. TSHM 235.3

Ndivyo itakavyotimilika utimilizo kamili wa ahadi ya maagano mapya: “Maana nitasamehe uovu wao, wala zambi yao sitakumbuka tena.” “Katika siku zile na wakati ule, anasema Bwana, uovu wa Israeli utatafutikana, wala uovu hapana; na zambi za Yuda zitafutikana, wala hazitaonekana.” “Na itakuwa, yeye aliyeachwa katika Sayuni, na yeye aliyebaki ndani ya Yerusalema, ataitwa mtakatifu, kila mmoja aliyeandikwa katika wale walio hai ndani ya Yerusalema.” Yeremia 31:34; 50:20; Isaya 4:3. TSHM 235.4