Go to full page →

Kufutia Mbali kwa Zambi TSHM 235

Kazi ya hukumu ya uchunguzi na kufutia mbali zambi inapashwa kutimizwa mbele ya kuja kwa Bwana mara ya pili. Katika huduma ya mfano kuhani mkuu alitoka inje na kubariki makutano. Vivyo hivyo Kristo, kwa mwisho wa kazi yake kama mpatanishi, ataonekana” si tena kwa zambi, lakini kwa wokovu.” Waebrania 9:28. TSHM 235.5

Kuhani, katika kuondoa zambi kutoka Pahali patakatifu, aliziungama juu ya kichwa mbuzi wa Azazeli. Kristo ataweka zambi hizi zote juu ya Shetani, mshawishi wa zambi. Mbuzi wa Azazeli akapelekwa mbali “katika inchi isiyo na watu.” Walawi 16:22. Shetani, katika kuchukua hatia za zambi alizolazimisha watu wa Mungu kuzifanya, atafungwa miaka elfu katika inchi isiyokaliwa kama jangwa na mwishoni atateswa kwa azabu ya moto utakaoangamiza waovu. Kwa hivi mpango wa wokovu utafikia utimilifu wake katika kungoa kwa mwisho kwa zambi. TSHM 235.6