Go to full page →

Kupimwa katika Mizani KN 209

Mungu huzipima tabia zetu, mwenendo wetu, na makusudi yetu kwa mizani ya patakatifu. Litakuwa jambo la kutisha kutajwa kwamba tumepungua katika upendo na utii kwa Mwokozi wetu, aliyekufa msalabani kuivuta mioyo yetu kwake. KN 209.2

Hasa wake wa wachungaji wetu wangekuwa waangalifu wasije wakayaasi mafundisho dhahiri ya Biblia juu ya jambo hili la zamani sana hata haina maana kuyajali; lakini Mwenye kuyatoa kwa wanafunzi wake alijua hatari zitokanazo na upendo wa mavazi katika siku zetu, akatupelekea onyo kubwa. Je, tutalitii onyo hili na kuwa wenye hekima? Upotevu wa mali katika mavazi huongezeka daima. Mwisho bado. Mtindo hubadilika kila mara, na akina dada huufuatilia, bila kujali wakati wala gharama. Fedha nyingi hutumiwa kwa mavazi, ambapo zingerudishwa kwa Mungu aliye Mtoaji. 64T 630, 631; KN 209.3