Go to full page →

Vitabu Vyenye kutia Mashaka Vilivyokatazwa na Mungu KN 239

Je, ni kusudi la Mungu kwamba mafundisho ya uongo, mawazo ya uongo, na madanganyo ya Shetani yawekwe mbele ya vijana na watoto wetu? Je, mashauri ama maono ya kishenzi na kikafiri yatolewe mbele ya wanafunzi wetu kama ongezeko la thamani la mafundisho yao? Vitabu vya akili za watu walio na mashaka sana ni vitabu vya hila mbaya zinazotumiwa kwa huduma va yule adui, yaani Shetani. Je, yawapasa wale ambao hufanya bidii kuwaongoa vizuri watoto na vijana katika njia sawa, katika njia waliyowekewa wateule wa Bwana kuifuata, wafikiri kuwa Mungu angependa wawafundishe vijana mambo yale ambayo yangeeleza vibaya tabia ya Mungu na kumsingizia? Hasha! 40CT.25,26 ; KN 239.1