Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Vita Kuu

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Sura Ya Kumi — Patakatifu

    *****

    FUNGU la Biblia ambalo limekuwa kama msingi wa nguzo ya imani juu ya kuja kwa Yesu zaidi ya mafungu vote, lilikuwa fungu lile linalosema: “Hata nyakati za jioni na asubuhi elfu mbili na mia tatu; ndipo patakatifu patakapotakaswa.” Dan. 8:14. Maneno haya yote yalijulikana na wote walioamini ya kuwa kuja kwa Bwana kulikuwa kumekaribia. Maneno haya ya unabii yalikaririwa kwa furaha na watu maelfu, tena yalikuwa kama kanuni ya imani yao. Wote walidhani ya kwamba matumaini yao yote valiyategemea mambo yaliyoonyeshwa katika fungu hili. Siku hizi za unabii zilizotajwa hapo, zilionyeshwa ya kwamba zingeishia mnamo 1844 katika siku za masika, kama mwezi wa Oktoba. Wale waliokuwa wakimngoja Yesu walikuwa wakifikiri mamoja na Wakristo wengine wote duniani, wakidhani ya kwamba dunia hii, au sehemu yake fulani, ndiyo iliyokuwa patakatifu, na ya kwamba kutakaswa kwa patakatifu ndiko kutakaswa kwa dunia na moto wa siku kuu ya mwisho. Walifahamu ya kwamba jambo hili litafanywa Kristo atakapokuja mara ya pili. Kwa hivyo wakakata neno ya kwamba Kristo atakuja duniani katika mwaka wa 1844.VK 76.1

    Lakini siku iliyowekwa iliwadia, wala Bwana hakuonekana. Waaminio walijua ya kwamba Neno la Mungu haliwezi kukosa; na bila shaka ni maelezo yao ya maneno ya unabii yasiyokuwa sawa; lakini kosa lilikuwa wapi? Wengi wao walikata shauri kwa haraka kwa kukanusha ya kwamba siku 2,300 ziliishia mnamo 1844. Hawakuweza kutoa sababu yo yote Wa kusema vile; isipokuwa walisema ya kwamba Kristo hakuja katika siku ile aliyotazamiwa. Walijadiliana wakisema ya kwamba kama siku zile za unabii zilitimia mnamo 1844, basi Kristo angalikuja kupatakasa patakatifu kwa kuitakasa dunia kwa moto; na ya kwamba kwa jinsi ambavyo hakuja, siku zile zilikuwa hazijatimia bado.VK 77.1

    Ingawa wingi wa wale waliomngoja Yesu waliacha njia yao ya zamani ya kuzihesabu nyakati za unabii, na baadaye waliukana usahihi wa mambo na mafundisho yaliyoegemezwa na unabii ule, kulikuwa na wachache kati yao waliokataa kuyakanusha mafundisho ya imani yao na mambo yaliyothibitishwa na neno la Biblia na shahidi maalum wa Roho wa Mungu. Waliamini ya kwamba katika kuchunguza maneno ya Biblia, walikuwa wamefuata njia za kweli kwa kueleza maneno yake, na ya kwamba ilikuwa wajibu wao kuyashikilia mafundisho ya kweli waliyokwisha kujifunza, na ya kwamba iliwapasa kudumu katika njia ile ile kwa kuchunguza maneno ya Biblia. Kwa maombi na juhudi waliyarudia mambo waliyokwisha kuyasoma, wakachunguza Biblia kwa uangalifu zaidi ill wapate kulivumbua kosa lao. Wasipoweza kuliona kosa katika maelezo yaliyotolewa juu ya nyakati za unabii, waliongozwa kuchunguza kwa makini sana yale mafundisho yanayohusiana na patakatifu.VK 77.2

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents