Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tumaini Kuu

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Ujumbe wa Wanafunzi Ukilinganishwa na Ujumbe wa Mwaka 1844

    Uzoefu walioupitia mitume kwenye ujio wa kwanza Wakristo ulipata kifani chake katika uzoefu wa wale walioutangaza ujio wake wa pili. Kama wanafunzi walivyohubiri wakisema, “Wakati umetimia, na ufalme wa Mungu umekaribia,” ndivyo Miller na wenzi wake walivyotangaza kwamba kipindi cha mwisho cha unabii wa Biblia kilikuwa kinakaribia kwisha, kwamba hukumu ya Mungu karibu, na kwamba ufalme wa milele ulikuwa unakaribia kuanza. Hotuba za wanafunzi kuhusu wakati zilikuwa zimejengwa katika majuma sabini ya Danieli 9. Ujumbe uliokuwa unatolewa na Miller pamoja na wanzi wake ulikuwa unatangaza mwisho wa siku 2300 za Danieli 8:14, ambazo ndani yake kuna yale majuma sabini. Mahubiri ya wanafunzi na akina Miller yalikuwa yanategemea kutimia kwa sehemu tofauti za unabii mmoja.TK 222.4

    Kama ilivyokuwa kwa wanafunzi wa kwanza, William Miller na wenzake hawakuuelewa kikamilifu ujumbe waliokuwa wanautoa. Makosa yaliyokuwa kanisani kwa muda mrefu yalizuia fasiri sahihi ya jambo muhimu katika unabii huo. Kwa hiyo, japo walikuwa wanatangaza ujumbe ambao Mungu alikuwa ameukabidhi kwao, lakini kutokana na fasili mbaya, waliishia kuvunjika moyo.TK 223.1

    Miller alichukua msimamo wa wengi kwamba dunia ndiyo “patakatifu” na akaamini kuwa “kutakaswa kwa patakatifu” kulikuwa kunawakilisha kutakaswa kwa dunia kwa moto wakati wa kuja kwa Bwana. Kwa hiyo alihitimisha kuwa mwisho wa zile siku 2300, ulikuwa unaonesha wakati wa ujio wa pili.TK 223.2

    Kutakaswa kwa patakatifu ilikuwa huduma ya mwisho iliyokuwa inafanywa na kuhani mkuu katika mzunguko wa kila mwaka. Ilikuwa sehemu ya mwisho ya upatanisho—kuhamisha na kuondoa dhambi katika Israeli. Ilikuwa inawakilisha kazi ya mwisho ya Kuhani wetu Mkuu huko mbinguni ya kuhamisha na kuondoa dhambi za watu wake zinazoandikwa katika vitabu vya mbinguni. Huduma hii inahusisha uchunguzi, yaani kuhukumu, nayo nafainyika kabla ya kurudi kwa Kristo akiwa katika mawingu, kwani atakapokuja kila kesi itakuwa imekwisha kuamuliwa. Yesu anasema: “Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.” Ufunuo 22:12. Kazi hii ya hukumu ndiyo inayotangazwa katika ujumbe wa malaika wa kwanza wa Ufunuo 14:7: “Mcheni Mungu, na kumtukuza, kwa maana saa ya hukumu yake imekuja.”TK 223.3

    Wale waliokuwa wanautangaza ujumbe huu walikuwa wanatoa ujumbe sahihi kwa wakati sahihi. Kama wanafunzi walivyokosea kuhusu ufalme uliokuwa usimamishwe mwishoni mwa yale “majuma sabini,” Waadventista nao walikosea juu ya tukio ambalo lingetokea mwishoni mwa zile “siku 2300.” Katika matukio yote, makosa yaliyokuwa yamezoeleka na wengi yalipofusha akili zisiuone ukweli. Wote walitimiza mapenzi ya Mungu katika kuuhubiri ujumbe aliokuwa anataka utolewe, na wote walivunjika moyo kutokana na kuuelewa vibaya ujumbe wao.TK 224.1

    Lakini Mungu alitimiza makusudi yake kwa kuruhusu onyo juu ya hukumu litolewe kama lilivyokuwa. Katika majaliwa yake, ujumbe huo ulikuwa wa kulipima na kulitakasa kanisa. Je, upendo wao ulikuwa umeelekezwa katika dunia hii au kwa Kristo na mbinguni? Je, walikuwa tayari kuachana na matamanio yao ya kidunia na kuukaribisha ujio wa Bwana wao?TK 224.2

    Kuvunjika kwa matumaini yao kulikusudiwa pia kupima mioyo ya wale waliokuwa wanadai kuwa wamepokea onyo hilo. Je, wangeiacha imani yao upesi na kuacha kuliamini Neno la Mungu wanapokutana na dhihaka ya ulimwengu na jaribu la kuchelewa na kuvunjika moyo? Je, wangeuacha ukweli uliothibitishwa na ushuhuda wa wazi wa Neno lake kwa sababu hawakuelewa upesi jinsi Mungu alivyokuwa anafanya kazi?TK 224.3

    Jaribio hili lingewaonesha hatari za kuchukua fasili za watu badala ya kuiacha Biblia ijifasili yenyewe. Wana wa imani wangepaswa kuisoma Biblia kwa makini, kuchunguza kwa undani misingi ya imani yao, na kukataa kila kitu ambacho hakikujengwa katika Maandiko, hata kama kinakubalika na wengi katika ulimwengu wa Kikristo.TK 224.4

    Jambo ambalo lilikuwa giza wakati wa kupimwa baadaye lingewekwa wazi. Pamoja na majaribu waliyoyapata kutokana na kukosea kwao, wangejifunza kupitia uzoefu wenye baraka kwamba Bwana ni “mwingi wa fadhili na kweli, kwao walishikao agano lake na shuhuda zake.” Zaburi 25:10.TK 224.5

    Unabii mrefu kuliko wote katika Biblia upo katika Danieli 8, ukifuatiwa na maelelezo zaidi katika Danieli 9. Unabii huu unaonesha wakati wa kusulibiwa kwa Kristo na mwanzo wa hukumu ya upelelezi kule mbinguni. Angalia Ukurasa 203-206TK 224.6

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents