Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    16 / KUTAFUTA UHURU KATIKA DUNIA MPYA

    Ijapo mamlaka na imani ya Roma mambo yale yalikataliwa, kanuni nyingi ziliingizwa katika ibada ya Kanisa la Uingereza. Ilidaiwa kwamba mambo yasiyokatazwa katika Maandiko hayakuwa na uovu wa hatari. Kwa kuyashika kunafaa kwa kupunguza shimo kubwa ambalo lilitenga makanisa ya matengenezo na Roma, na ilishurtishwa kwamba wangesaidia Wakatoliki kukubali imani ya Kiprotestanti.TSHM 136.1

    Kundi lingine halikuamua vile. Waliangalia desturi hizi kama dalili ya utumwa ambao walikombolewa. Walifikiri kwamba Mungu katika Neno lake ameimarisha maagizo kwa kutawala ibada yake, na kwamba watu hawana uhuru wa kuongeza kwa haya ao kutosha kwa haya. Roma ikaanza kulazimisha yale Mungu hakukataza,na ikaishia kukataza yale aliyo amuru wazi wazi.TSHM 136.2

    Wengi wakaangalia desturi za Kanisa la Kiingereza kama nguzo za ukumbusho wa ibada ya sanamu, na hawakuweza kujiunga kwa ibada yake. Lakini Kanisa lilisaidiwa na mamlaka ya serkali, haingeruhusu mafarakano. Mikutano isiyoruhusiwa kwa ajili ya ibada ilikatazwa chini ya malipizi ya kufungwa, kuhamishwa ao mauti.TSHM 136.3

    Kuwindwa, kuteswa, na kufungwa, watu walioishi maisha safi ya unyofu hawakuweza kutambua ahadi ya siku bora. Wengine wakakusudia kutafuta kimbilio katika Uhollande, wakasalitiwa katika mikono ya adui zao. Lakini wakavumilia kwa uaminifu na mwishowe wakashinda, na wakapata kimbilio katika pwani za urafiki.TSHM 136.4

    Waliacha nyumba zao na mali yao ya uchumi. Walikuwa wageni katika inchi ya kigeni, kurudia kwa kazi mpya ili wapate mkate wao. Lakini hawakupoteza wakati kwa uvivu ao kusikitika. Walimshukuru Mungu kwa ajili ya mibaraka waliyopata na wakawa na furaha katika ushirika wa kiroho wa raha ambao haukusumbuluwa.TSHM 136.5

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents