Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Imani lnayovumilia

    Wakati wa taabu na maumivu makuu yanayokuwa mbele yetu yatadai imani ile inayoweza kuvumilia ulegevu, kukawia, na njaa, imani ambayo haitalegea katika majaribu makali. Ushindi wa Yakobo ni ushuhuda wa nguvu ya maombi ya kushurutisha. Wote watakaoshikilia ahadi za Mungu, kama alivyofanya, watafaulu kama alivyofaulu. Kushindana na Mungu--namna gani wachache wanaojua umuhimu wake! Wakati mawimbi ya kukata tamaa yanapopita kwa nguvu juu ya mwombaji, namna gani wachache wanashikamana katika imani na ahadi za Mungu.TSHM 302.4

    Wale wanaotumia imani ndogo tu sasa wanakuwa katika hatari kubwa ya kuanguka chini ya mamlaka ya madanganyo ya Shetani. Na hata kama wanavumilia jaribu watatumbukia katika wasiwasi kubwa wakati wa taabu kwa sababu hawakuifanya kamwe kuwa zoezi la kumtumaini Mungu. Inatupasa sasa kutibitisha ahadi zake.TSHM 302.5

    Kila mara taabu ni kubwa linapofikiriwa aotendwa la mbele kuliko wakati ule kwa hakika linapashwa kutendeka ao kuonekana, lakini hii si kweli juu ya wakati wa taabu unaokuwa mbele yetu. Maelezo mengi ya wazi hayawezi kuikia ukubwa wa majaribu. Kwa wakati ule wa shida kila nafsi inapashwa kusimama yenyewe mbele ya Mungu.TSHM 303.1

    Sasa, wakati kuhani wetu Mkubwa anapofanya upatanisho kwa ajili yetu, inatupasa kutafuta kuwa wakamilifu katika Kristo. Si kwa wazo ambalo mwokozi wetu aliweza kuwezeshwa kujitoa kwa uwezo wa majaribu. Shetani anapata ndani ya mioyo ya kibinadamu mahali padogo ambapo anaweza kupata tegemeo la kusimamisha mguu; tamaa fulani ya zambi inatunzwa pale, na kwa njia ambayo majaribu yake kusimamia uwezo wao. Lakini Kristo anajitangaza mwenyewe: “Mkubwa wa dunia hii anakuja; na yeye hana kitu ndani yangu.” Yoane 14:30. Shetani hakuweza kupata kitu ndani ya Mwana wa Mungu ambacho kingeweza kumwezesha kupata ushindi. Hapakuwa zambi ndani yake ambayo Shetani angeweza kutumia kwa faida yake. Hii ni kawaida ambayo inapashwa kujitenga kwao watakaosimama katika wakati wa taabu.TSHM 303.2

    Ni katika maisha haya ambayo tunapashwa kujitenga na zambi, katika imani kwa damu ya Kristo ya upatanisho. Mwokozi wetu wa damani anatualika kujiunga kwake sisi wenyewe, kuunga uzaifu wetu kwa nguvu zake, kutostahili kwetu kwa matendo mema yake. Inabaki kwetu kushirikiana mbingu katika kazi ya kulinganisha tabia zetu kwa mfano wa Mungu.TSHM 303.3

    Kazi ya Shetani ya kudanganya na uharibifu itafikia kipimo cha juu (mwisho) wakatiwa taabu. Maono ya kuogofya ya tabia isiyokuwa ya kibinadamu karibu yatafunuliwa katika mbingu, kwa alama ya uwezo wa kazi za miujiza ya mashetani. Pepo wabaya wataendelea kwa “falme za dunia” na kwa ulimwengu wote, kuwashurtisha kuungana na Shetani katika mapigano yake ya mwisho juu ya serkali ya mbinguni. Watu watatokea kudai kuwa Kristo Mwenyewe. Watafanya maajabu ya kuponya na kujifanya kuwa na mambo ya ufunuo kutoka mbinguni kupinga Maandiko.TSHM 303.4

    Kama tendo la kutukuzwa katika ukubwa hadithi iliotungwamakusudi ya kuingizwa kama mchezo mbele ya watu wa madanganyo, Shetani mwenyewe atajifanya kuwa Kristo. Kanisa lilitazamia wakati mrefu kuja kwa Mwokozi kama utimilizo wa matumaini yake. Sasa mshawishi mkubwa atafanya kuonekana kwake ya kwamba Kristo amekuja. Shetani atajionyesha mwenyewe kama kiumbe chenye utukufu cha wangavu wa kushangaza, kufanana na sifa ya Mwana wa Mungu katika Ufunuo. Ufunuo 1:13-15.TSHM 303.5

    Utukufu unaomzunguka unapita kila kitu ambacho macho ya kibinadamu (wanaokufa) hayajaona kamwe. Shangwe ya ushindi italia, “Kristo amekuja!” Watu watamsujudia . Atanyosha mikono yake juu na kuwabariki. Sauti yake itakuwa ya kupendeza, lakini inapojaa na sauti tamu zinazofuatana. Kwa sauti ya huruma ataonyesha mambo mengine ya kweli ya ‘’mbinguni yaliotamkwa na Mwokozi. Ataponyesha magonjwa, na baadaye, katika tabia yake ya kujitia kwa mamlaka ya Kristo, anajidai kuweza kubadili Sabato na kuiweka kwa siku ya kwanza (dimanche). Anatangaza ya kwamba wale wanaoshika siku ya saba kuwa takatifu wanatukana jina lake. Hii ni madanganyo ya nguvu isiyoweza kuzuiwa na mtu. Watu wengi wanatoa usikizi kwa mambo haya ya uchawi, wakisema, Huu ni “uwezo mkubwa wa Mungu”, Matendo 8:10.TSHM 304.1

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents