Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Ujumbe Wa Malaika wa Kwanza

    Ujumbe wa malaika wa kwanza wa Ufunuo 14 ulitolewa kwa kutenga wale wanaojidai kuwa watu wa Mungu kutoka kwa mivuto mibaya. Katika ujumbe huu, Mungu alituma kwa kanisa onyo ambalo kama lingelikubaliwa, lingaliweza kusahihisha maovu ambayo yalikuwa yakiwafunga mbali na yeye. Kama wangalikubali ujumbe, kushusha mioyo yao na kutafuta matayarisho kwa kusimama mbele yake, Roho wa Mungu angalionekana. Kanisa lingalifikia tena umoja ule, imani, na upendo wa siku za mitume, wakati waaminifu “walikuwa na moyo mmoja” na wakati “Bwana aliongezea kwa kanisa kila siku wale waliokuwa wakiokolewa.” Matendo 4:32; 2:47.TSHM 181.4

    Kama watu wa Mungu wangalipokea nuru kutoka kwa Neno lake, wangalifikia umoja ule ambao mtume anaeleza, “umoja wa Roho katika kifungo cha salama”. Anasema, “Mwili ni mmoja, na Roho mmoja, kama vile mulivyoitwa katika tumaini moja la mwito wenu; Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja.” Waefeso 4:3-5.TSHM 182.1

    Wale waliokubali ujumbe wa kurudi kwa Yesu walikuja kutoka makanisa mbalimbali, na vizuizi vyao vya dini vikatupwa chini kwa nguvu. Kanuni za imani za mabishano zikavunjika kwa vipande vipande. Maoni ya uwongo juu ya kuja kwa mara ya pili yakasahihiswa. Makosa ya kanyoshwa, mioyo ikaungana katika upatano wakupendeza. Upendo ukatawala sana. Mafundisho haya yangefanya vile kwa wote, kama wote wangelikubali.TSHM 182.2

    Wahuduma, ambao kama walinzi walipashwa kuwa wa kwanza kutambua dalili za kuja kwa Yesu, walishindwa kujifunza ukweli kutoka kwa manabii ao kwa ishara za wakati. Upendo kwa Mungu na imani katika Neno lake vikapunguka, na mafundisho juu ya kurudi kwa kristo ikaamsha tu kutokuamini kwao. Kama kwa zamani ushuhuda wa Neno la Mungu ukakutana na swali: “Nani katika wakubwa ao Wafarisayo aliyemwamini?” Yoane 7:48. Wengi walipinga majifunzo ya unabii, kufundisha kwamba vitabu vya unabii vilitiwa muhuri na havikuwa vya kufahamika. Makundi, kwa kutumainia wachungaji wao, wakakataa kusikiliza; na wengine, ingawa walisadikishwa na ukweli, hawakusubutu kukiri ili wasipate “kutoshzwa katika sunagogi.” Yoane 9:22. Ujumbe Mungu alioutuma kwa kujaribu kanisa ulionyesha namna gani watu walikuwa wengi waliotia mapendo yao kwa dunia hii kuliko kwa Kristo.TSHM 182.3

    Kukataa maonyo ya malaika wa kwanza kulisababisha na hali ya kutisha ya tabia ya kupenda anasa ya kidunia, kuacha dini, na mauti ya kiroho ambayo yalikuwa katika makanisa katika mwaka 1844.TSHM 182.4

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents