Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Kuinua Pazia Kwa Wakati Ujao

    Mbele ya kuingia kwa zambi, Adamu alipendezwa na ushirika wazi na Muumba wake; lakini tangu mtu alipojitenga mwenyewe na Mungu kwa njia ya uasi, taifa la kibinadamu likakatiliwa mbali na bahati hii kubwa. Kwa shauri la ukombozi, walakini, njia ilifunguka ambayo kwayo wakaaji wa dunia wanaweza tena kuwa na uhusiano na Mungu. Mungu aliongea pamoja na watu kwa njia ya Roho yake, na nuru ya kimungu ilitolewa kwa walimwengu kwa njia ya ufunuo kwa watumishi wake wateule. “Watu walisema yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na Roho Mtakatifu.” 2 Petro 1:21.TSHM iii.1

    Wakati miaka ya kwanza ya 2500 ya historia ya mwanadamu, hapakuwa na ufunuo ulioandikwa. Wale waliokuwa wakifundisha mambo ya Mungu walitoa habari zao kwa wengine, na zilipokelewa kutoka kwa baba na kwa mtoto, hata kwa vizazi vilivyofuatana. Matayarisho ya neno lililoandikwa yalianza kwa wakati wa Musa. Ufunuo ulioongozwa na Mungu ndipo ukapata kuwekwa katika kitabu cha Uongozi wa Mungu. Kazi hii ikaendelea kwa muda mrefu wa miaka 1600-tangu wakati wa Musa mwandishi wa historia ya kuumbwa na sheria, hata kwa wakati wa Yoane, mwandishi wa mambo ya kweli na bora zaidi ya injili.TSHM iii.2

    Biblia huonyesha Mungu kama Mtengenezaji wa kitabu hicho; ingawa kiliandikwa na mikono ya wanadamu; na kwa namna mbalimbali ya vitabu vyenye kuachana huonyesha tabia za waandishi kadha wa kadha. Mambo ya kweli yaliyofunuliwa yote “limepewa kwa maongozi ya Mungu” 2 Timoteo 3:16; lakini yalielezwa katika maneno ya watu. Yeye asiye na mwisho kwa Roho wake Mtakatifu alitoa nuru kwa akili na mioyo ya watumishi wake. Alitoa ndoto na maono, mifano na sanamu; na hao ambao kweli ilifunuliwa kwao wakaweka wao wenyewe wazo katika msemo wa kibinadamu.TSHM iii.3

    Viliandikwa katika nyakati mbalimbali, kwa watu walioachana sana katika cheo na kazi, na katika karama za akili na roho, vitabu vya Biblia vinaonyesha sura pana za kuachana, pia na tofauti katika hali ya vita vinavyonenwa bila kuelezwa. Aina mbambali ya maelezo yalitumiwa na waandishi mbalimbali; mara kwa mara ukweli huo huo unakuwa wa kushangaza zaidi ulipotolewa na mojawapo kuliko mwengine. Na kwa namna waandishi wengi wanavyo fundisha fundisho kwa mifano mbalimbali na mahusiano, hapo panaweza kutokea, mambo ya juu juu, ya ovyo ovyo, ao msomaji mwenye kupendelea, kuwa tofauti wala mabishano, ambaye mwanafunzi wa heshima, na maoni wazi, hutambua asili ya umoja. TSHM iii.4

    Kama ilivyoonyeshwa kwa watu mbalimbali, ukweli umeletwa katika sura zake mbalimbali. Mwandishi mmoja anaweza kutiwa moyo kwa nguvu kwa kipande kimoja cha fundisho; anashika nikta ambazo zinapatana na ujizi wake ao uwezo wake wa kufahamu na shukrani; mwengine hushikilia kwa hali tofauti yake; na kila mmoja, chini ya uongozi wa Roho Mtakatifu, hutoa kitu kinachotia moyo kwa nguvu kwa ajili yake mwenyewe-hali mbalimbali ya ukweli katika kila mmoja, lakini umoja kamili katika mambo yote. Na kweli zilizo funuiiwa hujiunga kufanya kitu kizima kamili, kinacholingana kukutana na shida za watu katika mambo yote na ujuzi wa maisha.TSHM iv.1

    Mungu amependezwa kujulisha ukweli wake ulimwenguni kwa njia ya watu wajumbe, naye mwenyewe, kwa njia ya Roho wake Mtakatifu, watu wanaofaa na aliwawezesha kufanya kazi hii. Aliongoza akili katika uchaguzi wa mambo gani ya kusema na mambo gani ya kuandika. Hazina zilikabidhiwa kwa vyombo vya kidunia, lakini ni hivyo, kupana kitu kilichotoka mbinguni. Ushuhuda umetolewa kwa maneno zaifu ya lugha ya kibinadamu, lakini ni ushuhuda wa Mungu; na mtoto mtiifu, mwenye kuamini wa Mungu hushika ndani yake utukufu wa uwezo wa Mungu, amejaa neema na kweli.TSHM iv.2

    Katika Neno lake, Mungu ameweka maarifa yake ya lazima kwa watu kwa wokovu. Maandiko Matakatifu yanafaa kukubaliwa kama ufunuo wenye nguvu, na wenye hakika ya mapenzi yake. Yanakuwa kanuni ao kipeo cha tabia yake, mvumbuaji wa mafundisho ya dini, na jaribu la maarifa. “Kila andiko limepewa kwa pumzi ya Mungu, na linafaa kwa mafundisho, na kwa kuonya watu juu ya makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa mafundisho katika haki; ili mtu wa Mungu awe mukamilifu, ametengenezwa kabisa kwa kila tendo jema.” 2 Timoteo 3:16, 17.TSHM iv.3

    Lakini ingawa Mungu amefungua mapenzi yake kwa watu kwa njia ya Neno lake, jambo hili halikufanya jambo lisilotakiwa kwa kuwako kwake kuendelea na kuongoza kwa Roho Mtakatifu. Kwa kinyume, Roho iliahidiwa na Mwokozi wetu, kwa kufungua Neno kwa watumishi wake, kwa kuangazia na kutumia mafundisho yake. Na kwa sababu ilikuwa Roho ya Mungu iliyoongoza Biblia, haiwezekani kwamba mafundisho ya Roho ilipaswa kuwa kinyume kwa mafundisho ya Neno.TSHM iv.4

    Roho haikutolewa-ama hata kuwekwa-kwa kutangua Biblia; kwa maana Maandiko hueleza wazi wazi kwamba Neno la Mungu ni kipao ambacho mafundisho yote na ujuzi yanapaswa kujaribiwa. Asemavyo mutume Yoane, “Musiamini kila roho, lakini jaribuni roho, kama zimetoka kwa Mungu; kwa sababu manabii wengi wa uwongo wametokea duniani.” 1 Yoane 4:1. Na Isaya husema, “Kwa sheria na kwa ushuhuda! Kama hawasemi sawasawa na neno hili, kweli hapana asubui kwao.” Isaya 8:20.TSHM iv.5

    Laumu kubwa liliwekwa juu ya kazi ya Roho Mtakatifu kwa makosa ya aina ya wale, wanaodai mwangaza wake, wanaoungama kuwa na kutokuwa na haja zaidi tena ya uongozi kutoka kwa Neno la Mungu. Wanatawaliwa na maoni ambayo wanayozania kama sauti ya Mungu katika roho. Lakini roho ile inayowaongoza si Roho ya Mungu. Hii kwa kufuata maoni, kwa kutojali Maandiko, kunaweza kuongoza kwa machafuko tu, kwa udanganyifu na maangamizi. Hutumia tu makusudi zaidi ya yule muovu. Hivi kazi ya Roho Mtakatifu inakuwa ya maana sana kwa uzima wa kanisa la Kristo, ni mojawapo kati ya mashauri ya Shetani, kwa njia ya makosa ya wanaozidisha mambo kupita na washupavu kwa kutia zarau juu ya kazi ya Roho na kuletea watu wa Mungu kutojali asili ya nguvu ambayo Bwana wetu Mwenyewe ameitoa.TSHM v.1

    Katika mapatano pamoja na Neno la Mungu, Roho yake ilikuwa kwa kuendelea kazi yake katika muda wote wa mgawo wa injili. Kwa mda wa miaka wakati Maandiko ya Agano la Kale na Agano Jipya yalikuwa yakitolewa, Roho Mtakatifu hakuacha kutoa nuru kwa roho za watu, isipokuwa mafunuo kuwekwa katika Sheria Takatifu. Biblia yenyewe inahubiri namna gani, kwa njia ya Roho Mtakatifu, watu walipokea maonyo, kemeo, shauri, na mafundisho, katika mambo katika kukosa namna kwa kuhatidia kwa kutolewa kwa Maandiko. Manabii walitajwa wa nyakati mbalimbali, ambao maneno yao hakuna yaliyoandikwa. Na kumbukumbu lilifanywa hivyo, baada ya kufungwa kwa sheria ya Maandiko, Roho Mtakatifu alikuwa wakuendelea kazi yake, kwa kuangazia, kuonya, na kufariji waana wa Mungu.TSHM v.2

    Yesu aliahidi wanafunzi wake, “Mufariji, Roho Mtakatifu, ambaye Baba atakayemutuma kwa jina langu, yeye atawafundisha ninyi yote, na kuwakumbusha ninyi yote niliyowaambia ninyi.” “Lakini wakati anapokuja yule Roho ya kweli, atawaongoza ninyi katika yote yaliyo kweli... naye atawatangazia ninyi habari za maneno yatakayokuja.” Yoane 14:26; 16:13. Maandiko yanafundisha wazi wazi kwamba ahadi hizi, hazikuwekewa mpaka kwa siku za mitume tu, zitaenea kwa kanisa la Kristo katika miaka yote. Mwokozi anaahidi wafwasi wake, “Mimi ni pamoja nanyi siku zote hata mwisho wa dunia.” Matayo 28:20. Na Paulo anasema kwamba zawadi na mafunuo ya Roho yaliwekwa katika kanisakwa ukamilifu wa watakatifu, kwa kazi ya hudumu ili mwili wa “Kristo ujengwe; hata sisi sote tufikie umoja wa imani, na kujua sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu muzima, hata kufika kipimo cha urefu wa utimilifu wa Kristo.” Waefeso 4:12, 13.TSHM v.3

    Kwa ajili ya waaminifu wa Efeso mtume aliomba, “Ili Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa utukufu, awape ninyi Roho ya hekima na wa ufunuo katika kumjua yeye; macho ya ufahamu wenu yatiwe nuru ili mujue tumaini la kuita kwake, ... na ukubwa wa kupita wa uwezo wake kwetu tunaoamini.” Waefeso 1:17-19. Kazi ya huduma ya Roho wa Mungu katika kuangazia ufahamu na kufungua roho kwa vitu vingi vya Neno Takatifu la Mungu ilikuwa ndiyo baraka ambao Paulo aliomba sana kwa ajili ya kanisa la Waefeso.TSHM vi.1

    Baada ya mafunuo ao maonyesho ya ajabu ya Roho Mtakatifu kwa Siku ya Pentekote, Petelo akaonya watu kwa ajili ya toba na ubatizo katika jina la Kristo, kwa ondoleo la zambi zao; na alisema: “Nanyi mutapokea zawadi ya Roho Mtakatifu. Kwa sababu ahadi ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu.” Matendo 2:38, 39.TSHM vi.2

    Katika uhusiano na gafula pamoja na tendo za siku kuu ya Mungu, Bwana kwa njia ya nabii Yoeli ameahidi ufunuo wa kipekee wa Roho Mtakatifu. Yoeli 2:28. Unabii huu ulipata sehemu ya utimilizo katika kumiminika kwa Roho siku ya Pentekote; lakini itafikia utimilizo wake kamili katika ufunuo wa neema ya Mungu ambao utafuatana na kufungwa kwa kazi ya injili, vita kuu kati ya mema na mabaya itaongezeka kwa mkazo kwa mwisho kabisa wa wakati. Katika miaka ya hasira ya Shetani ilionekana juu ya kanisa la Kristo; na Mungu ameweka neema yake na Roho kwa watu wake kwa kuwatia nguvu kusimama kwa kupinga uwezo wa yule muovu. Wakati mitume wa Kristo walipashwa kupeleka injili yake duniani na kuiandika kwa ajili ya miaka yote ijayo, walipata karama ya kipekee ya mwangaza wa Roho. Lakini kwa namna kanisa linapokaribia ukombozi wake wa mwisho, Satana atatumika na uwezo mwingi. Ameshuka chini “mwenye hasira nyingi kwa sababu anajua ana wakati mufupi tu.” Ufunuo 12:12. Atatumika “na uwezo wote, na alama na maajabu ya uwongo.” 2 Watesalonika 2:9. Kwa miaka 6000 yule mwerevu mara alikuwa juu sana miongoni mwa malaika wa Mungu amegeuka kabisa kwa kazi ya madanganyifu na maangamizi. Na vina vya ustadi wa Shetani na ujanja alioupata, ujanja wote uliositawishwa wakati wa taabu ya miaka italetwa kwa kuchukuliwa juu ya watu wa Mungu katika vita ya mwisho. Na katika wakati huu wa hatari wafwasi wa Kristo watapaswa kuchukua duniani maonyo ya kuja kwa mara ya pili kwa Bwana; na watu watapaswa kujitayarisha kusimama mbele yake kwa kuja kwake, “pasipo waa wala laumu.” 2 Petro 3:14. Kwa wakati huu matoleo ya kipekee ya neema ya Mungu na uwezo haikose kuhitajiwa kwa kanisa kuliko katika siku za mitume.TSHM vi.3

    Kwa njia ya mwangaza wa Roho Mtakatifu, tendo za vita yenye kuendelea wakati mrefu kati ya mema na mabaya vimefunguliwa kwa mwandishi wa kurasa hizi. Mara kwa mara nimeruhusiwa kutazama matengenezo ama kazi, katika miaka mbali mbali ya maisha, ya vita kuu kati ya Kristo, Mfalme wa uzima, Muumba wa wokovu wetu, na Shetani, mfalme wa uovu, asili ya zambi, muasi wa kwanza wa sheria takatifu ya Mungu. Uadui wa Shetani juu ya Kristo umeonekana juu ya wafuasi wake. Uchuki wa namna moja wa kanuni za sheria ya Mungu, mashauri ya namna moja ya udanganyifu, ambaye kosa limefanyika kuonekana kama kweli, ambaye sheria za kibinadamu zimebadilika kuwa pahali pa sheria ya Mungu, na watu wameongozwa kuabudu kiumbe kuliko Muumba, yapate kuandikwa katika historia yote ya wakati uliopita. Nguvu za Shetani kwa kusingizia tabia ya Mungu, kwa kulazimisha watu kutunza wazo la uongo la Muumba, na hivyo kumzania na hofu na uchuki kuliko kuwa na upendo; juhudi yake kwa kuweka pembeni sheria ya Mungu, kuongoza watu kufikiri wao wenyewe kuwa na uhuru kwa matakwa yake; na mateso yake ya wale wanaothubutu kupinga hila zake, imefuatiwa kwa bidii sana katika miaka yote ya maisha. Yameweza kuandikwa katika historia ya wazee wakuu (patriarches), manabii, na mitume, ya wafia dini na watengenezaji.TSHM vii.1

    Katika vita kuu ya mwisho, Shetani atatumia maongozi ya namna moja, kuonyesha roho ya namna moja, na kutumikia mwisho wa namna moja kama katika miaka yote iliyotangulia. Kile kilichokuwa, kitakuwa, isipokuwa kwamba taabu itakayokuja itafahamika na mkazo wa kutisha sana ambako dunia haijashuhudia. Madanganyo ya Shetani yatakuwa ya ujanja zaidi, mashambulio yake ya gafula yatakuwa ya makusudi zaidi. Kama ikiwezekana, angeongoza kwa kupoteza wachaguliwa. Marko 13:22.TSHM vii.2

    Namna Roho ya Mungu ilivyofungua roho yangu mambo ya kweli makubwa ya Neno lake, na vitendo vya wakati uliopita na vya wakati ujao, nimeagizwa kujulisha wengine mambo yale yaliyo funiliwa-kwa kuandika historia ya vita katika miaka iliyopita, na hasa zaidi kwa kuitoa kama kutawanya nuru juu ya taabu inayokaribia upesi ya wakati ujao. Kwa kufuata kusudi hili, nimejitahidi kuchagua na kukusanya pamoja mambo katika historia ya kanisa kwa namna hii, ili kuandika yasiyo funuliwa ya majaribu makubwa ya kweli ambayo kwa nyakati mbali mbali yametolewa ulimwenguni, yale yaliyoamsha hasira ya Shetani na uadui wa kanisa la upendo wa kidunia, na yale yaliyoshikwa kwa ushuhuda wa wale “wasiopenda maisha yao hata kufa.”TSHM vii.3

    Katika kumbusho hizi tunaweza kuona kivuli cha vita mbele yetu. Kwa kuzitazama katika nuru ya Neno la Mungu, na mwangaza wa Roho yake, tunaweza kuona kufunuliwa kwa mashauri ya waovu na hatari wanazopashwa kuepuka yule angeweza kupatikana “bila kuwa na kosa” mbele ya Bwana wakati wa kuja kwake.TSHM viii.1

    Matukio makubwa yaliyoonyesha maendeleo ya matengenezo katika miaka iliyopita yanakuwa mambo ya historia, yanayojulikana sana na kukubaliwa pote na ulimwengu wa Kiprotestanti; yanakuwa hakika ambayo hakuna mtu anaweza kuyakana. Historia hii niliyotolewa kwa kifupi, kwa kupatana na kusudi la kitabu na uchache wa maneno utakaochunguzwa, kweli kwamba kilipunguzwakuwa kidogo kinavyoonekana kwa kulingana sawa na ufahamu kamili wa matumizi yake. Katika mambo mengine mahali msimulizi amekusanya matukio pamoja kama kwa kutoa, kwa kifupi, maoni ya ufahamu wa fundisho, ao maelezo ya muhitasari wa kutaja kila kitu katika namna inayofaa, maneno yake yameingizwa; lakini kwa mara mengine hakuna sifa njema kabisa imetolewa, kwa kuwa mateuzi (quotations) hayakutolewa kwa ajili ya kusudi la kutaja mwandishi yule kuwa mwenye mamlaka, lakini maneno yake hutoa zawadi ya rahisi na ya hodari ya mafundisho. Katika kusumulia maarifa na maoni ya wale wanaoendelea kuchukua kazi ya matengenezo katika wakati wetu wenyewe, matumizi ya namna moja yamefanywa kwa kazi zao za kutangaza.TSHM viii.2

    Si zaidi sana kusudi la kitabu hiki kutoa mambo ya kweli mapya kwa ajili ya taabu za nyakati za kwanza kwa kutoa mambo na kanuni zinazokuwa na sura ya matukio yanayokuja. Kwani inaonekana kama sehemu ya vita kati ya nguvu za nuru na giza, hodari hizi zote za kumbukumbu za wakati uliopita zinaonekana kuwa na maana mpya; na kati yake nuru inatiwa juu ya wakati ujao, kuangazia njia ya wale, wanaopenda watengenezaji (reformateurs) wa miaka iliyopita, wataitwa, hata kwa hatari ya hali njema ya kidunia, kushuhudia “kwa ajili ya neno la Mungu, na kwa ajili ya ushuhuda wa Yesu Kristo.”TSHM viii.3

    Kwa kueleza tendo za vita kuu kati na ukweli na uongo; kwa kufunua hila za Shetani na makusudi ambayo angeweza kufaulu kushindana nayo; kutoa suluhu la kufanyikiwa kwa shida kuu ya uovu, kugawanya nuru ya namna hiyo juu ya tabia ya asili na ya mwisho ya zambi kama kufanya ufunuo kamili wa haki na wema wa Mungu katika mambo yake yote pamoja na viumbe vyake; na kuonyesha hali takatifu, isiyo badilika ya sheria yake, ndilo lengo la kitabu hiki. Ili kwa mvuto wake roho ziweze kukom`bolewa kutoka kwa uwezo wa giza na kuwa “washiriki wa urithi wa watakatifu katika nuru,” kwa sifa ya Yeye aliyetupenda na alijitoa mwenyewe kwa ajili yetu ni ombi la moyo la mwandishi.TSHM ix.1

    Ellen G. White

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents