Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Wenye Mashaka na Wasioamini

    Kristo alisema kwamba kama vile watu wa siku za Noa “hawakujua hata garika ilipokuja na kuwaondosha wote; ndivyo kutakavyokuwa kuja kwa Mwana wa watu.” Matayo 24:39. Wakati watu wanaojidai kuwa watu wa Mungu wanapojiunga pamoja na dunia, wakati anasa ya dunia inakuwa anasa ya kanisa, wakati wote wanapotazamia miaka nyingi ya mafanikio ya kidunia--ndipo, kwa gafula kama nuru ya umeme, utakuja mwisho wa matumaini yao ya uongo. Kama vile Mungu alivyotuma mtumishi wake kwa kuonya dunia juu ya kuja kwa Garika, ndivyo alivyotuma wajumbe waliochaguliwa kujulisha ukaribu wa hukumu ya mwisho. Na kama watu wa wakati wa Noa walichekelea kwa kuzarau ubashiri wa muhubiri wa haki, ndivyo hivyo katika siku za Miller wengi kati ya wale wanaojidai kuwa watu wa Mungu wakachekelea maneno ya maonyo.TSHM 161.3

    Hapo hapakuwa tena na ushahidi wa mwisho wakuonyesha kwamba makanisa yalitoka kwa Mungu kuliko machukio yaliyoamshwa na ujumbe huu uliotumwa na Mungu.TSHM 161.4

    Wale waliokubali mafundisho ya kuja waliona kwamba ilikuwa wakati wa kukamata msimamo. “Mambo ya umilele yakawa kwao kitu cha kweli. Mbingu ililetwa karibu, na walijiona wao wenyewe kuwa na kosa mbele za Mungu.” Wakristo walifanywa kuona kwamba wakati ulikuwa karibu, mambo walipashwa kutendea wenzao yalipaswa kufanywa kwa upesi. Umilele ulionekana kufunguliwa mbele yao. Roho wa Mungu alitoa uwezo kwa miito yao kujitayarisha kwa ajili ya siku ya Mungu. Maisha yao ya siku kwa siku ilikuwa mi laumu kwa washiriki wa kanisa wasiotakaswa. Hawa hawakutaka kusumbuliwa katika furaha yao, kutafuta feza, na tamaa ya nguvu kwa ajili ya heshima ya kidunia. Ndipo wakapinga imani ya kiadventisti.TSHM 161.5

    Wapinzani wakajitahidi kupinga uchunguzi kwa kufundisha kwamba mambo ya unabii yalitiwa muhuri. Kwa hiyo Waprotestanti wakafuata nyayo za washiriki wa kanisa la Roma. Makanisa ya Waprotestanti wakadai kwamba sehemu kubwa ya Maandiko matakatifu--yale yanayotoa nuru kwa Neno la Mungu, sehemu ile inayofaa zaidi kwa wakati wetu, haikuweza kufahamika. Wachungaji wakasema kwamba Danieli na Ufunuo vilikuwa vitabu vya siri isiyoweza kufahamika kwa wanadamu.TSHM 162.1

    Lakini Kristo aliongoza wanafunzi wake kwa maneno ya nabii Danieli, “Yeye anayesoma afahamu.” Matayo 24:15. Na kitabu cha Ufunuo kinapaswa kufahamika. “Ufunuo wa Yesu Kristo aliopewa na Mungu aonyeshe watumishi wake maneno yaliyopaswa kuwa upesi... Heri anayesoma nao wanaosikia maneno ya unabii huu, na kushika maneno yaliyoandikwa ndani yake; kwa maana wakati ni karibu.” Ufunuo 1:1-3, matoleo ya herufi za italics.TSHM 162.2

    “Heri anayesoma” kunakuwa na wale hawatasoma; na “nao wanaosikia” hapo kuna wengine wanaokataa kusikia kitu cho chote juu ya mambo ya unabii; “na kusikia maneno yaliyoandikwa ndani yake” wengi wanakataa kusikia mafundisho katika Ufunuo; hakuna kati ya hawa anayeweza kudai mibaraka iliyoahidiwa.TSHM 162.3

    Namna gani watu husubutu kusingizia kwamba Ufunuo ni siri inayopita fahamu ya wanadamu? Ni siri iliyofunuliwa, kitabu kilichofunuliwa. Ufunuo unaongoza mawazo kwa Danieli. Wote wawili wanaonyesha mafundisho makubwa juu ya mambo makubwa kwa mwisho wa historia ya dunia.TSHM 162.4

    Yoane aliona hatari, vita, na kukombolewa kwa mwisho kwa watu wa Mungu. Aliandika mambo ya ujumbe wa mwisho unaopasa kukamilisha mavuno ya dunia, au kwa gala la mbinguni au kwa moto wa uharibifu, ili wale wanaogeuka kutoka kwa mabaya hata kwa ukweli waweze kufundishwa juu ya hatari na mapigano yanayo kuwa mbele yao.TSHM 162.5

    Sababu gani, basi, juu ya ujinga huu unaoenea sana juu ya sehemu kubwa hii ya Maandiko matakatifu? Ni matokeo ya juhudi iliyokusudiwa ya mfalme wa giza kwa kuficha watu yale yanayofunua madanganyifu yake. Kwa sababu hii, Kristo Bwana wa Ufunuo huu, kwa kuona mbele ya wakati vita juu ya fundisho la Ufunuo, akatangaza baraka kwa wote watakaoweza kusoma, kusikia, na kushika unabii. TSHM 163.1

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents