Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    34 / NI WANANI WANAOKUWA “PEPO” KATIKA IMANI YA ROHO ZA WATU WALIOKUFA HURUDI NA KUJIONYESHA NA KUONGEA NA WATU?

    Mafundisho ya maisha ya milele ya kawaida, mara ya kwanza yaliletwa kutoka kwa hekima ya kishenzi na katika giza ya maasi makubwa yaliyounganishwa katika imani ya Kikristo, yakaondosha kweli ambayo “wafu hawajui kitu.” Muhubiri 9:5. Wengi wanaamini ya kwamba pepo za wafu ni “roho za kutumikia, zilizotumwa kutumikia wale watakaoriti wokovu.” Waebrania 1:14.TSHM 269.1

    Imani ya kwamba roho za wafu zinarudi kutumia walio hai ikatayarisha njia kwa imani ya wafu ya kisasa kuwa roho za watu waliokufa hurudi kujionyesha na kuongea na watu. Kama wafu wanakuwa na majaliwa na maarifa inayopita zaidi ile waliyokuwa nayo mbele, sababu gani kutorudi duniani na kufundisha wa hai? Kama roho za wafu zinatangatanga kwa rafiki zao duniani, sababu gani hazipelekane habari nao? Namna gani wale wanaoamini katika uaminifu wa kibinadamu katika mauti wanaweza kukana “nuru ya Mungu” iliyotolewa na roho tukufu? Hapa kuna mferezi unaoweza kuangaliwa kama takatifu ambamo shetani anatumika. Malaika walioanguka wanaonekana kama wajumbe kutoka ulimwengu wa kiroho.TSHM 269.2

    Mfalme wa mabaya anakuwa na uwezo wa kuleta mbele ya watu mfano wa rafiki waliokufa. Mfano ni kamilifu, ulifatishwa kwa uzahiri wa ajabu. Wengi wanafarijika na hakikisho ya kwamba wapenzi wao wana furaha mbinguni. Bila mashaka ya hatari, wanatoa sikio kwa roho za kudanganya, na mafundisho ya mashetani.” 1 Timoteo 4:1.TSHM 269.3

    Wale waliokwenda kwa kaburi bila kujitayarisha wanadai kuwa na furaha na kuwa mahali pa cheo bora huko mbinguni. Wageni wa uwongo kutoka kwa ulimwengu ya mapepo (spirits) mara ingine hutoa maonyo halisi yanayoshuhudia kuwa hakika. Halafu, kwa hivi tumaini linapatikana, wanafundisha mafundisho yale yanayongoa Maandiko. Kwa sababu kwamba wanataja mambo mengine ya kweli na palepale kutabiri mambo ya wakati ujao jambo hilo linatoa mfano wa hakika, na mafundisho yao ya uwongo yanakubaliwa. Sheria ya Mungu huwekwa kando, Roho ya neema huzarauliwa. Pepo wanakana Umungu wa Kristo na wanaweka Muumba kwa cheo pamoja na wao wenyewe.TSHM 269.4

    Wakati inakuwa kweli kwamba matokeo ya udanganyifu mara kwa mara yamepokewa kwa hila kama maonyesho ya kweli, pale kulikuwa, vilevile, maonyesho ya kupambanua ya uwezo wa ajabu, kazi kabisa ya malaika waovu. Wengi wanaamini ya kwamba imani yakuwa roho za watu waliokufa hurudi na kujionyesha na kuongea na watu ni ujanja tu wa kibinadamu. Kama ikiletwa mbele ya maonyesho ambayo hawawezi kuizania namna ingine isipokuwa kama ni ya ajabu, watadanganyiwa na kuyakubali kama uwezo mkubwa wa Mungu.TSHM 270.1

    Kwa msaada wa Shetani wachawi wa Farao wakaiga kazi ya Mungu. Tazama Kutoka 7:10-12. Paulo anashuhudia kwamba kuja kwa Bwana kutatanguliwa na “kutenda kwa Shetani na uwezo wote, na ishara na maajabu ya uwongo”. 2 Watesalonika 2:9,10. Na Yoane anatangaza: “Naye anafanya mastaajabu makubwa, hata kufanya moto kushuka toka mbingu juu ya dunia, mbele ya watu. Naye anawakosesha wale wanaokaa juu ya dunia, kwa mastaajabu yale aliyopewa kufanya. Ufunuo 13:13, 14. Si mambo ya ujanja tu yaliyotabiriwa hapa. Watu wanadanganyiwa na mastaajabu ambayo wajumbe wa Shetani wanafanya, si yale wanayotaka kufanya.TSHM 270.2

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents