Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Wakati wa Taabu ya Yakobo

    Peke yake pamoja na Mungu, akaungama zambi zake kwa unyenyekevu sana. Taabu katika maisha yake ilifika. Katika giza akaendelea kuomba. Gafula mkono ukawekwa juu ya bega lake. Akafikiri kwamba adui ndiye alikuwa akitafuta maisha yake. Kwa nguvu zote za kukata tamaa akapigana kwa nguvu na adui wake. Wakati siku ilipoanza kucha, mgeni akatumia nguvu zisizokuwa za kibinadamu. Yakobo akaonekana kukauka na akaanguka, muombaji zaifu, mwenye kulia kwa shingo la mshindani wake wa siri. Akajua nyuma ya kwamba alikuwa malaika wa agano aliyekuwa akigombana naye. Alidumu katika majuto wakati mrefu kwa ajili ya zambi yake; sasa anapashwa kuwa na matumaini ya kwamba alisamehewa. Malaika akasihi sana, “Uniache niende, ni mapambazuko”, lakini mzee mkuu akapandisha sauti, “Sitakuacha kwenda mpaka utakaponibariki”. Yakobo akaungama uzaifu wake na kutostahili kwake, huku akatumainia rehema za Mungu mwenye kulinda maagano. Kwa njia ya toba na kujitoa, kiumbe hiki cha mauti na mwenye zambi akashindana na Mtukufu wa mbinguni.TSHM 300.2

    Shetani akamshitaki Yakobo mbele ya Mungu kwa sababu ya zambi yake; akashawishi Esau kusafiri na kinyume chake. Wakati wa usiku wa mzee mkuu wa kushindana, Shetani akajaribu kumkatisha tamaa na kuvunja tumaini lake kwa Mungu. Alivutwa karibu kukata tamaa; lakini akatubu kwa kweli juu ya zambi yake na kushikilia Malaika imara nakaendelea na maoni yake pamoja na vilio vya juhudi hata akashinda.TSHM 301.1

    Kwa namna Shetani alivyomshitaki Yakobo, ataendelea na masitaka yake juu ya watu wa Mungu. Anakuwa na taarifa sahihi ya zambi alizokuwa wakiwajaribu nazo kutenda na anatangaza ya kwamba kwa haki hawezi kuwasamehe zambi zao kwani kumwangamiza na malaika zake. Anadai ya kwamba watolewe mikononi mwake kuangamizwa.TSHM 301.2

    Bwana anamruhusu kuwajaribu iwezekanavyo. Tumaini lao kwa Mungu, imani yao, itajaribiwa kwa ukali. Wanapo jikumbusha yalipopita, imani yao inazama, kwani kwa maisha yao yote wanaweza uzuri ndogo. Shetani anajaribu kuwatisha kwa mafikara kuwa kezi zao hakuna matumaini. Anatumaini pia kuharibu imani yao ili wajitoe kwa majaribu na kugeuza utii wao kutoka kwa Mungu.TSHM 301.3

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents