Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Si Mapenzi ya Mungu

    Haikuwa mapenzi ya Mungu kwamba Israeli azunguke zunguke miaka makumi ine jangwani; alitamani kuwaongoza mara moja kwa Kanana na kuwaimarisha kule, watu watakatifu na wafuraha. Lakini “hawakuweza kuingia kwa sababu ya kutokuamini kwao.” Waebrania 3:19. Ni namna ileile, haikuwa mapenzi ya Mungu kwamba kuja kwa Kristo kupate kuchelewa wakati mrefu na watu wake wadumu miaka mingi sana duniani hii ya zambi na huzuni. Kutoamini kukawatenga kwa Mungu. Katika rehema kwa ulimwengu, Yesu akakawisha kuja kwake, ili wenye zambi wasikie onyo na kupata kimbilio kabla ya hasira ya Mungu kumiminika.TSHM 221.3

    Sasa kama katika vizazi vya kwanza, kutangazwa kwa ukweli kutaamsha upinzani. Wengi kwa kijicho wanashambulia tabia na makusudi ya wale wanaosimama katika kutetea ukweli usiopendwa na wengi. Elia alitangazwa kuwa mwenye kuleta taabu katika Israeli. Yeremia msaliti, Paulo mwenye kuchafua hekalu. Tangu siku ile hata leo, wale ambao wangekuwa waaminifu kwa kweli wameshitakiwa kuwa kama wafitini, wajushi, ao wenye kutengana.TSHM 221.4

    Kukiri kwa imani kulikofanywa na watakatifu na wafia dini, mifano hiyo ya utakatifu ukamilifu imara, kunatia moyo ndani ya wale wanaoitwa sasa kusimama kama washahidi kwa ajili ya Mungu. Kwa mtumishi wa Mungu kwa wakati huu kunaagizo linalosema: “Paza sauti yako kama baragumu, uhubiri watu wangu kosa lao, na nyumba ya Yakobo zambi zao.” “Nimekuweka kuwa mlinzi kwa nyumba ya Israeli; kwa hivi sikia neno kwa kinywa changu, na uwape maonyo toka kwangu.” Isaya 58:1; Ezekieli 33:7.TSHM 222.1

    Kizuizi kikubwa kwa kukubali kweli ni kwamba inahusika na taabu na laumu. Hii ni mabishano tu kinyume cha ukweli ambayo wateteaji wake hawakuweza kamwe kupinga. Lakini wafuasi wa kweli wa Kristo hawangojei ukweli kukubaliwa na watu wengi. Wanakubali msalaba, pamoja na Paulo kuhesabu kwamba “Mateso yetu mepesi yaliyo kwa dakika tu, yanatufanyia utukufu wa milele unaouzito mwingi”; pamoja na mmoja wa zamani, “akihesabu ya kuwa kulaumiwa kwa Kristo ni utajiri mwingi kuliko hazina za Misri.” 2 Wakorinto 4:17; Waebrania 11:26.TSHM 222.2

    Inatupasa kuchagua haki kwa sababu inakuwa haki, na kuacha matokeo kwa Mungu. Kwa watu wa kanuni, imani na uhodari, dunia inakuwa na deni kwa ajili ya matengenezo yake makubwa. Kwa watu wa namna ile kazi ya matengenezo kwa wakati huu inapashwa kuendelea mbele.TSHM 222.3

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents