Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Utakaso ni Nini?

    Maelezo yenye makosa juu ya utakaso pia yanaonekana kwa kutojali wala kukana kwa sheria ya Mungu. Maelezo haya, ya uwongo katika mafundisho na ya hatari katika matokeo ya maisha, kwa kawaida yanapata kibali.TSHM 226.5

    Paulo anatangaza, “Maana haya ni mapenzi ya Mungu, hata utakaso wenu.” Biblia inafundisha wazi wazi utakaso ni nini na namna gani unaweza kufikiwa. Mwokozi aliombea wanafunzi wake: “Uwatakase kwa kweli; neno lako ni kweli.” Na Paulo anafundisha kwamba waaminifu wanapashwa “kutakaswa na Roho Mtakatifu.’‘ 1 Watesalonika 4:3; Yoane 17:17; Waroma 15:16.TSHM 227.1

    Kazi ya Roho Mtakatifu ni nini? Yesu akawambia wanafunzi wake: “Lakini wakati anapokuja yule Roho wa kweli, atawaongoza ninyi katika yote yaliyo kweli.” Yoane 16:13. Na mwandishi wa Zaburi anasema: “Sheria yako ni ya kweli.” Kwa hivi sheria ya Mungu ni “takatifu na ya haki na njema,” tabia iliyofanywa kwa utii kwa sheria ile itakuwa takatifu. Kristo aliye mufano kamili wa tabia ya namna ile Anasema: “Nimeshika amri za Baba yangu.” “Ninafanya saa zote mambo yanayomupendeza.” Yoane 15:10; 8:29. Wafuasi wa Kristo wanapaswa kuwa kama yeye--kwa neema ya Mungu kufanya tabia katika umoja pamoja na kanuni za sheria yake takatifu. Huu ni utakaso wa Biblia.TSHM 227.2

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents