Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Kipimo cha Hukumu

    Sheria ya Mungu ni kipimo katika hukumu. “Ogopa Mungu, na shika amri zake; maana maneno haya ni yote inayofaa mtu kufanya. Kwa maana Mungu ataleta kila kazi hukumuni.” “Semeni ninyi, na kutenda kama watu watakaohukumiwa kwa sheria ya uhuru.” Muhubiri 12:13,14; Yakobo 2:12.TSHM 233.3

    Wale “wanaohesabiwa kuwa wamestahili” watakuwa na sehemu katika ufufuko wa wenye haki, Yesu akasema: “Lakini wale watakaohesabiwa kuwa wamestahili kupata dunia ile na kufufuka kutoka wafu,... ni wana wa Mungu, wakiwa wana wa ufufuo.” “Wale waliofanya mema watafufuka kwa ufufuko wa uzima.” Luka 20:35,36; Yoane 5:29. Wafu wenye haki hawatafufuliwa hata baada ya hukumu ambayo watakayohesabiwa kuwa wamestahili kwa “ufufuo wa uzima.” Kwa sababu hiyo hawatakuwako katika nafsi wakati vilivyoandikwa juu ya vingali na chunguzwa kesi zao kukatwa.TSHM 233.4

    Yesu atatokea kama mwombezi wao, kutetea kwa ajili yao mbele ya Mungu. “Na Kama mtu yeyote akitenda zambi, tunaye Mwombezi kwa Baba, Yesu Kristo mwenye haki.” “Kwa sababu Kristo hakuingia katika Pahali patakatifu palipofanywa kwa mikono, ndio mfano wa kweli, lakini aliingia mbinguni zenyewe, aonekane sasa mbele ya Mungu kwa ajili yetu.” “Naye, kwa sababu hii anaweza pia kuwaokoa wanaokuja kwake Mungu kwa njia yake; maana yeye ni hai siku zote apate kuwaombea.” 1 Yoane 2:1; Waebrania 7:25; 9:24.TSHM 234.1

    Wakati vitabu vya ukumbusho vinapofunguliwa katika hukumu, maisha ya wote walioamini kwa Yesu yanakuja katika ukumbusho mbele ya Mungu. Kuanzia kwa wale walioishi kwanza duniani, Mtetezi wetu anaonyesha kesi za kila kizazi kwa kufuatana. Kila jina linatajwa, kila kesi inachunguzwa. Majina yanakubaliwa, majina yanakataliwa. Wakati mtu ye yote anakuwa na zambi zinazodumu kwa vitabu vya ukumbusho, zisizoungamwa na kusamehewa, majina yao yatafutwa katika kitabu cha uzima. Bwana akamwambia Musa: “Mutu aliyenikosea, ndiye nitakayemwondosha katika kitabu changu.” Kutoka 32:33.TSHM 234.2

    Wote waliotubu kwa kweli na katika imani wakadai damu ya Kristo kama kafara yao ya upatanishi walipata rehema wakaingia katika vitabu vya mbinguni. Kwa namna wanafanywa washiriki wa haki wa Kristo na tabia zao zinaonekana kuwa katika umoja na sheria ya Mungu, zambi zao zitafutwa mbali, na watahesabiwa wenyekustahili uzima wa milele. Bwana anasema: “Mimi, ndiye anayefuta makosa yako kwa ajili yangu mwenyewe; nami sitakumbuka zambi zako.” “Yeye anayeshinda atavikwa nguo nyeupe, wala sitaondosha jina lake katika kitabu cha uzima; nami nitakiri jina lake mbele ya Baba yangu, na mbele ya malaika zake.’‘ “Basi kila mtu anayenikiri mbele ya watu, nitamukiri vilevile mbele ya Baba yangu aliye mbinguni.” Isaya 43:25; Ufunuo 3:5; Matayo 10:32,33.TSHM 234.3

    Mtetezi wa kimungu anaonyesha maombi yale yote ya walioshinda kwa njia ya imani katika damu yake wapate kurudishwa kwa makao yao ya Edeni na kuvikwa taji kama kuwa wariti pamoja naye mwenyewe kwa “mamlaka ya mwanzo.” Mika 4:8. Sasa Kristo anauliza ya kuwa mpago wa kimungu katika kuumbwa kwa mtu upate kutimizwa kama kwamba mtu hakuanguka kamwe. Anauliza kwa ajili ya watu wake si rehema tu na kuhesabiwa haki, bali sehemu katika utukufu wake na kukaa kwa kiti chake cha enzi.TSHM 234.4

    Wakati Yesu anapoombea watu neema yake, Shetani anawashitaki mbele ya Mungu. Anaonyesha ukumbusho wa maisha, upungufu wa tabia, kuwa na tofauti kwa Kristo, kwa zambi zote alizowajaribu nazo kufanya. Kwa sababu ya mambo haya anawadai kuwa watu wake.TSHM 235.1

    Yesu haruhusu zambi zao, lakini anaonyesha toba yao na imani. Anapoomba msamaha kwa ajili yao, anainua mikono yake iliyojeruhiwa mbele ya Baba, kusema: Nimewachora kwa viganja vya mikono yangu. “Zabihu za Mungu ni roho ya kuvunjika, moyo uliovunjika na toba hutauzarau, Ee Mungu.” Zaburi 51:17.TSHM 235.2

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents