Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Choyo lliyofichwa Imefunuliwa

    Mambo yote ya ukaidi wa choyo iliyofichwa yamefunuliwa katika vitabu vya mbinguni. Mara ngapi wakati, mawazo, na nguvu zinazokuwa za Kristo zilitolewa kwa Shetani. Wafuasi wa Kristo wanashughulika katika upataji wa mali ya kidunia ao furaha ya anasa ya ulimwengu. Mali, wakati, na nguvu zinatumiwa kwa maonyesho na anasa; nyakati za bidii kwa kuomba ni chache, kwa kutafuta Maandiko, kuungama zambi.TSHM 236.4

    Shetani anavumbua mashauri mengi yasiyohesabika kwa kutumia mawazo yetu. Mdanganyi mkubwa anachukia mambo makubwa ya kweli yale yanayoonyesha kafara ya upatanisho na Mpatanishi hodari. Kwake kila kitu kinategemea juu ya kugeuza mawazo kutoka kwa Yesu.TSHM 236.5

    Wale wanaoweza kugawa faida ya upatanisho wa Mwokozi hawapaswi kuruhusu kitu cho chote kujiingiza kwa shughuli yao kukamilisha utakatifu katika kumcha Mungu. Saa za damani, badala ya kuzitoa kwa anasa ao kwa kutafuta faida, zinapashwa kutolewa kwa kujifunza katika maombi kwa Neno la Kweli. Pahali patakatifu na hukumu ya uchunguzi vinapaswa kufahamiwa wazi. Wote wanahitaji ujuzi wa cheo na kazi ya Kuhani wao Mkuu. Kama sivyo itakuwa haiwezekani kutumia kanuni ya imani kwa wakati huu.TSHM 237.1

    Mahali patakatifu huko mbinguni ndipo pahali Kristo anaweka shabaha ya kazi kwa ajili ya wanadamu. Hii ni kwa kila roho inayoishi duniani. Inafungua kwa maoni mpango wa wokovu, kutuleta chini kwakufungwa kwa kukataa kati ya ukamilifu na zambi.TSHM 237.2

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents