Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Uchuki Ukasitawishwa Katika Uasi wa Juhudi

    Mungu katika hekima yake akaruhusu Shetani kuendelea na kazi yake, hata roho ya uchuki ikasitawishwa katika uasi. Ilikuwa ni lazima kwa mashauri yake kuendelea kabisa, ili tabia yake ya kweli iweze kuonekana kwa wote. Lusifero alikuwa mwenye kupendwa sana na viumbe vya mbinguni, na mvuto wake juu yao ulikuwa wa nguvu. Serkali ya Mungu haikuhusikana tu na wakaaji wa mbinguni, lakini kwa dunia zote alizoziumba; na Shetani akafikiri kwamba kama akiweza kuchukua malaika pamoja naye katika uasi, angeweza kuchukua vilevile dunia zingine. Kutumia madanganyo na werevu, uwezo wake kwa kudanganya ulikuwa mkubwa sana. Hata Malaika waaminifu hawakuweza kabisa kutambua tabia yake wala kuona ni kitu gani kazi yake ilikuwa ikiongoza.TSHM 241.4

    Shetani alikuwa akiheshimiwa sana, na matendo yake yote kuvikwa sana na siri, mpaka ilikuwa vigumu kuonyesha kwa malaika tabia ya kweli ya kazi yake. Hata ilipositawi kabisa, zambi haikuonyesha kitu kibaya kilichokuwako. Viumbe vitakatifu havikuweza kutambua matokeo ya kuweka kando sheria ya Mungu. Shetani mwanzoni alisema alikuwa anatafuta kuendelesha heshima ya Mungu na uzuri wa wakaaji wote wa mbinguni.TSHM 242.1

    Katika mipango yake juu ya zambi, Mungu aliweza kutumia tu haki na kweli. Shetani aliweza kutumia mambo ambayo Mungu hakuweza kutumia--uongo na werevu. Tabia ya kweli ya mnyanganyi ilipashwa kufahamiwa na wote. Alipashwa kuwa na wakati kujionyesha mwenyewe kwa kazi zake za uovu.TSHM 242.2

    Ugomvi ambao alianzisha yeye mwenyewe mbinguni, Shetani aliuwekea juu ya Mungu. Uovu wote aliutangaza kuwa matokeo ya utawala wa Mungu. Kwa hiyo ilikuwa ni lazima kwamba aonyeshe wazi matokeo ya makusudi yake ya kugeuza sheria ya Mungu. Kazi yake mwenyewe ilipashwa kumuhukumu. Viumbe vyote vya ulimwengu vilipashwa kuona mdanganyi kufunuliwa.TSHM 242.3

    Hata wakati ilipokusudiwa kwamba hawezi tena kudumu mbinguni, Mungu wa hekima isiyokuwa na mwisho hakumuangamiza Shetani. Utii wa viumbe vya Mungu unapashwa kuwa juu ya sadikisho la haki yake. Wakaaji wa mbinguni na wa dunia zingine, walipokuwa bila kujitayarisha kufahamu matokeo ya zambi, hawakuweza basi kuona haki na rehema ya Mungu katika maangamizi ya Shetani. Kama angaliangamizwa mara moja, wangemtumikia Mungu kwa hofu kuliko kwa upendo. Mvuto wa mdanganyi haungeharibiwa kabisa, wala roho ya uasi kungolewa kabisa. Kwa faida ya viumbe vyote katika vizazi vyote, Shetani alipashwa kuendelesha kabisa kanuni zake, kwamba mashambulio yake juu ya mamlaka ya Mungu yapate kuonekana katika nuru yake ya kweli kwa viumbe vyote vilivyoumbwa.TSHM 242.4

    Uasi wa Shetani ulipashwa kuwa kwa viumbe vyote ushuhu- da kwa matokeo ya kuogopesha ya zambi. Kanuni yake ingeonyesha matunda ya kuweka kando mamlaka ya Mungu. Historia ya tendo hili la kuogopesha la uasi lilipashwa kuwa ulinzi wa milele kwa akili takatifu zote kuwaokoa kwa zambi na kwa azabu yake.TSHM 242.5

    Wakati ilipotangazwa kwamba pamoja na washiriki wake wote mnyanganyi mkubwa wa ufalme anapashwa kufukuzwa kutoka kwa makao ya cheo cha furaha, mwongozi muasi (mhuni) akatangaza wazi bila woga zarau kwa ajili ya sheria ya Muumba. Akalaumu sheria za Mungu kama kizuio cha uhuru na akatangaza kusudi lake la kupata kuondoshwa kwa sheria. Kwa kuwekwa huru kwa amri hii, majeshi ya mbinguni wangeweza kuingia juu ya hali ya kujipandisha zaidi katika maisha.TSHM 243.1

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents