Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    20 / UPENDO KWA AJILI YA KUJA KWA KRISTO

    6Uamsho mkubwa wa dini umetabiriwa katika ujumbe wa malaika wa kwanza wa Ufunuo 14. Malaika moja ameonekana akiruka “katikati ya mbingu, mwenye Habari Njema ya milele, ahubiri kwao wanaokaa juu ya dunia, na kila taifa na kabila na lugha na jamaa.” “Kwa sauti kubwa” akatangaza: “Ogopeni Mungu, na kumutukuza kwa maana saa ya hukumu yake imekuja. Mukamwabudu yeye aliyefanya mbingu na dunia na bahari na chemchemi za maji.” Ufunuo 14:6,7.TSHM 170.1

    Malaika ni mfano wa tabia bora ya kazi inayopaswa kutimizwa kwa ujumbe na uwezo na utukufu, ambavyo vinapaswa kuishugulikia. Kuruka kwa malaika “katikati ya Mbingu,” “sauti kubwa,” na matangazo yake “kwa kila taifa na kabila na lugha na jamaa” inatoa ushuhuda wa kuenea kwa upesi, katika dunia nzima kwa tendo. Kwa habari ya wakati ambao inapaswa kufanyika, inatangaza kufunguliwa kwa hukumu.TSHM 170.2

    Ujumbe huu ni sehemu ya habari njema (injili) ambayo ingeweza kutangazwa tu katika siku za mwisho, ambapo tu ndipo inaweza kuwa hatika kwamba saa ya hukumu yake imekuja. Sehemu ile ya unabii wake ambao inaelekea kwa siku za mwisho, Danieli aliagizwa kufunga na kutia muhuri “hata wakati wa mwisho.” Danieli 12:4. Mpaka wakati huu ndipo ujumbe juu ya hukumu utangazwe, wenye msingi na kutimilika kwa unabii.TSHM 170.3

    Paulo alionya kanisa lisitazamie kuja kwa Kristo katika siku zake. Mpaka baada ya uasi mkubwa na utawala mrefu wa “mtu wa zambi” tunaweza kutazamia kuja kwa Bwana wetu. Tazama 2 Watesalonika 2:3. “Mtu wa zambi” vilevile “siri ya uasi,” “mwana wa uharibifu,” na “yule mwenye uovu,” ni mfano wa cheo cha Papa, ambacho kilikuwa kwa kushikilia mamlaka yake kwa miaka 1260. Mda huu ulimalizika kwa mwaka 1798. Kuja kwa Kristo hakungefanyika mbele ya wakati ule. Paulo anaeneza onyo lake kwa ile inayohusu Wakristo wote hata kwa mwaka 1798. Kwa upande huu wa wakati ule, ujumbe wa Kuja kwa Kristo mara ya pili ukatangazwa. Sivyo ujumbe wa namna ile haujatolewa kamwe kwa vizazi vilivyopita. Paulo, kama tulivyoona, hakuuhubiri; aliuweka mbali kwa wakati ujao ujumbe wa kuja kwa Bwana. Watengenezaji hawakuutangaza. Martin Luther aliweka siku ya hukumu karibu ya miaka 300 zijazo kutoka kwa siku zake. Lakini tangu 1798 kitabu cha Danieli kilifunuliwa, na wengi wakatangaza ujumbe wa hukumu kuwa karibu.TSHM 170.4

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents