Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Roger Williams

    Kama vile Wasafiri wa kwanza, Roger Williams akaja kwa Dunia Mpya kufurahia uhuru wa dini. Lakini aliufahamu kwa namna ingine si kama Wasafiri, akaona mambo ambayo watu wachache tu waliona, kwamba uhuru huu ulipashwa kuwa haki kwa watu wote. Alikuwa mtafuti (atafutaye) wa bidii wa kweli. Williams alikuwa mtu wa kwanza katika Ukristo wa kisasa kwa kuanzisha serkali inayosimamia kwa mafundisho ya uhuru wa zamiri.” “Watu ao waamuzi wanaweza kukata shauri,” akasema, “ni nini inastahili kati ya mtu na mtu; lakini wanapojaribu kufafanua wajibu wa mtu kwa Mungu, hapa wanaachana na Mungu, na hapo hapawezi kuwa na salama; kwani ni wazi kwamba kama mwamuzi anakuwa na uwezo, angeweza kuamuru shauri fulani ao imani leo na ingine kesho; kama ilivyokuwa ikifanyika katika Uingereza na wafalme wa kuachana na wamalkia, na mapapa wa kuachana na mabaraza katika Kanisa la Roma.”TSHM 138.1

    Kuhuzuria katika kanisa lililosimamishwa ililazimishwa chini ya malipo ao kifungo. “Kushurutisha watu kuungana pamoja na wale wa imani ya kuachana, yeye (Williams) aliangalia jambo hilo kama kutendea zambi kwa wazi kwa haki zao halisi, kukokota watu wasio kuwa wa dini kwa ibada na wasiopenda, ilikuwa ni kukuza unafiki... Hakuna mutu alipashwa kulazimishwa kuabudu Mungu, ao, akaongeza, kushikilia ibada, kinyume cha ukubali wake mwenyewe!”TSHM 138.2

    Roger Williams aliheshimiwa, lakini haja yake kwa ajili ya uhuru wa dini haukuweza kuvumiliwa. Kwa kuepuka kufungwa akalazimishwa kukimbilia kati kati ya baridi ng zoruba ya majira ya baridi katika poli usiokatwa bado.TSHM 138.3

    “Kwa muda wa majuma kumi na inne,” akasema, “Nikarushwa sana katika majira ya uchungu, bila kuwa na mkate ao kitanda.” Lakini “Kunguru wakanilisha jangwani,” shimo ndani ya mti nikaitumia mara kwa mara kuwa ficho.” Akaendelea na ukimbizi wake wa uchungu katika theluji na mwitu usio na njia hata akapata kimbilio pamoja na kabila la Wahindi ambao aliopata matumaini na upendo wao.TSHM 138.4

    Akaweka msingi wa jimbo la kwanza la nyakati za kisasa lile lililo tambua haki “kwamba kila mutu alipashwa kuwa na uhuru kwa kuabudu Mungu kufuatana na nuru ya zamiri yake mwenyewe.” Jimbo lake ndogo, Kisiwa cha Rhode, likaongezeka na kusitawi hata kwa kanuni zake za msingi--uhuru wa serekali na wa dini--vikawa mawe ya pembeni ya Jamuhuri ya Amerika.TSHM 138.5

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents