Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    3 / GIZA LA KIROYO KATIKA KANISA LA KWANZA

    Mtume Paulo alisema kwamba siku ya Kristo haingepaswa kuja “ila maasi yale yafike mbele, na mtu yule wa kuasi akafunuliwe, mwana wa uharibifu, yeye mpinzani na kujionyesha mwenyewe juu ya yote yanayoitwa Mungu ao kuabudiwa, hata kuketi ndani ya hekalu la Mungu akijionyesha mwenyewe kama yeye ndiye Mungu”. Na zaidi, “Maana siri ya uasi hata sasa inatenda kazi”. 2 Watesalonika 2:3,4,7. Hata kwa tarehe ile ya mwanzo mtume aliona, makosa kuingia kimya polepole, yale yangetayarisha njia kwa ajili ya Kanisa la Kipapa.TSHM 14.1

    Pole pole, “siri ya uasi” ikaendesha kazi yake ya Kudanganya. Desturi za kipagani zikapata njia zao katika kanisa la Kikristo, zilipozuiwa wakati wa mateso makali chini ya upagani; lakini wakati mateso yalipokoma, ukristo ukaweka kando unyenyekevu wa Kristo kwa ajili ya fahari ya mapadri wa kipagani na watawala. Kugeuka kwa jina tu kwa Constantini ukaleta furaha kubwa. Sasa kazi ya maovu ikaendelea kwa upesi. Upagani, ulionekana kushindwa kabisa.. Mafundisho yake na mambo ya uchawi yakaingia katika imani ya waliojidai kuwa wafuasi wa Kristo.TSHM 14.2

    Mapatano haya kati ya upagani na ukristo yakatokea katika “mutu wa zambi” aliyetabiriwa katika unabii. Dini ile ya uwongo kazi bora ya Shetani, juhudi yake kwa kukaa mwenyewe juu ya kiti cha ufalme kwa kutawala dunia kufuatana na mapenzi yake.TSHM 14.3

    Ni mojawapo ya mafundisho ya Kiroma ya msingi kwamba Papa amepewa mamlaka kuu juu ya maaskofu na wachungaji (pasteurs) katika ulimwengu wote. Zaidi ya jambo hili ameitwa “Bwana Mungu Papa” na ametangaziwa kuwa asiyeweza kukosa. (Tazama Mwisho wa Kitabu (Nyongezo)) Madai ya namna moja yallazimishwa na Shetani katika jangwa la majaribu yangali yakiendeshwa naye kati ya Kanisa la Kirumi, na hesabu kubwa wanamtolea heshima kubwa.TSHM 14.4

    Lakini wale wanaoheshimu Mungu wanapigana majivuno haya kama vile Kristo alipambana na adui mwerevu: “Utaabudu Bwana Mungu wako,yeye peke utamutumikia”. Luka 4:8. Mungu hakuagiza kamwe mtu ye yote kuwa kichwa cha kanisa. Utawala wa kipapa unakuwa kinyume kabisa na Maandiko. Papa hawezi kuwa na mamlaka juu ya Kanisa la Kristo isipokuwa kwa njia ya kunyanganya. Warumi huleta juu ya Waprotestanti madai ya kwamba kwa mapenzi yao walijitenga kwa kanisa la kweli. Lakini ni wao waliacha “imani waliyopewa watakatifu mara moja tu”. Yuda 3.TSHM 14.5

    Shetani alijua vizuri kwamba ilikuwa kwa Maandiko matakatifu ambayo Mwokozi alishindana na mashambulio yake. Kwa kila shambulio, Kristo alionyesha ngabo ya kweli ya milele, kusema, “Imeandikwa”. Kwa kudumisha uwezo wa utawala wake juu ya watu na kuanzisha mamlaka ya Papa munyanganyi, anapaswa kuendelea kufunga, watu katika kutojua Maandiko matakatifu. Mambo ya kweli matakatifu yake yalipaswa kufichwa na komeshwa. Kwa mda wa miaka mamia ya uenezaji wa Biblia ulikatazwa na Kanisa la Roma. Watu wakakatazwa kuisoma. Mapadri na waaskofu wakatafsiri mafundisho yake kwa kuendesha madai yao. Kwa hiyo Papa akajulikana pote kama msaidizi wa Mungu ulimwenguni.TSHM 15.1

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents