Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Mda wa Nyakati Mbili Zilianza Pamoja

    Lakini kukatiliwa mbali kwa nini? Hivi siku 2300 zilikuwa ni mda tu wa wakati uliotajwa katika sura 8, majuma makumi saba yanapaswa basi kuwa sehemu ya siku 2300. Nyakati mbili hizo zinapaswa kuanza pamoja, majuma makumi saba tangu “kuwekwa amri” ya kutengeneza na kujenga Yerusalema. Kama tarehe ya amri hii ingeweza kupatikana, ndiyo ingekuwa mwanzo wa uhakika wa siku 2300.TSHM 155.3

    Katika sura ya saba ya Ezra amri inapatikana, ilitolewa na Artasasta, mfalme wa Persia, katika mwaka 457 B.C. Wafalme watatu katika kuanzisha na kutimiza amri, wakaifanya kwa utimilivu uliotakiwa na unabii kwa kutia alama ya mwanzo wa mwaka 2300. Kukamata miaka 457 B.C., wakati amri ilipotimia, kama tarehe ya “amri”, kila hatuwa ya majuma makumi saba ikaonekana katika kutimilika. (Tazama Nyongezo.)TSHM 155.4

    Kwa kuendelea kwa kutengeneza na kujenga Yerusalema hata Masiya Mfalme itakuwa majuma saba, na majuma makumi sita na mawili”majuma makumi sita na kenda, ao miaka 483. Amri ya Artasasta ikatendeka katika wakati wa masika wa mwaka 457 B.C. Kutoka tarehe hii, miaka 483 ikafikia kwa wakati wa masika wa mwaka 27 A.D. Kwa wakati ule unabii huu ukatimilika. Katika wakati wa masika wa mwaka 27 A.D.Kristo akabatizwa na Yoane na akapakwa mafuta ya Roho. Baada ya ubatizo wake akaenda Galilaya, “akihubiri Habari njema ya ufalme wa Mungu akisema: Wakati umetimia.” Marko 1:14, 15.TSHM 155.5

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents