Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Ulinzi wa kweli Kabisa wa Ukuu wa Taifa

    Kanuni za Biblia zilikuwa zikifundishwa katika jamaa, chuoni, na kanisani; matunda yake yalionekana katika uangallifu wa kutumia feza, akili, usafi, na kiasi. Mtu mmoja angeweza kwa muda wa miaka “bila kuona mlevi, ao kusikia kiapo, wala kukutana na muombaji.” Kanuni za Biblia ndizo kingo ao walinzi wa kweli kabisa wa ukuu wa taifa. Inchi zaifu zilizokuwa chini ya utawala wa inchi ingine (colony) zilifanikiwa na kuwa majimbo yenye uwezo, na dunia ikaona usitawi wa “kanisa bila Papa, na serkali bila mfalme.”TSHM 139.5

    Lakini hesabu iliongezeka ya watu waliovutwa na Amerika kwa makusudi tofauti na Wasafiri wa kwanza. Hesabu iliyoongezeka ni ya wale waliotafuta tu faida ya kidunia.TSHM 139.6

    Mabwana wa kwanza wakaruhusu washiriki wa kanisa tu kwa kuchagua ao kuongoza kazi katika Serkali. Mpango huu ulikubaliwa kwa kulinda usafi wa Serkali; ukaleta matokeo ya uharibifu wa kanisa. Wengi wakajiunga na kanisa bila badiliko la moyo. Hata katika kazi ya injili kulikuwa wale waliokuwa wajinga wa uwezo mpya wa Roho Mtakatifu. Tangu siku za Constantine hata wakati huu, kujaribu kujenga kanisa kwa usaada wa serkali, ambapo inaweza kuonekana kuleta ulimwengu karibu ya kanisa, kwa kweli huleta kanisa karibu ya ulimwengu.TSHM 139.7

    Makanisa ya Protestanti ya Amerika, na yale ya Ulaya pia, yakashindwa kuendelea mbele katika njia ya matengenezo. Wengi, kama Wayahudi wa siku za Kristo ao wakatoliki katika wakati wa Luther, walirizika kuamini kama mababa zao walivyoamini. Makosa na ibada ya sanamu vilishikwa. Matengenezo polepole yakafa, hata kukawa haja kubwa sana ya matengenezo katika makanisa ya Kiprotestanti hata katika kanisa la kiRoma wakati wa Luther. Hapo kulikuwa heshima ya namna moja kwa maoni ya watu na kutia mafikara ya binadamu kwa nafsi ya Neno la Mungu. Watu wakaacha kutafuta Maandiko na kwa hiyo wakaendelea kutunza mafundisho ambayo haikuwa na msingi katika Biblia.TSHM 140.1

    Kiburi na upotovu (ujinga) yakalindwa chini ya umbo la dini, na makanisa yakaharibika. Mambo ya asili ambayo yalipaswa kuharibu mamilioni ya watu yalikuwa yakipata mizizi ya nguvu. Kanisa lilikuwa likishika mambo ya asili haya baadala ya kushindana kwa ajili ya “imani ambayo iliyotolewa kwa watakatifu.”TSHM 140.2

    Ndiyo namna kanuni ziliunguzwa heshima (aibishwa) ambazo Watengenezaji walizotesekea sana. TSHM 140.3

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents