Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Mwito kwa Kuabudu Muumba

    Wajibu kwa kuabudu Mungu unaimarishwa juu ya kweli kwamba yeye ni Muumba. “Kujeni, tuabudu na kuinama; Tupige magoti mbele ya Bwana mwenye kutuumba.” Zaburi 95:6; Tazama Zaburi 95:5; Zaburi 100:3; Isaya 40:25,26; 45:18.TSHM 210.5

    Katika Ufunuo 14, watu wameitwa kuabudu Muumba na kushika amri za Mungu. Mojawapo ya amri hizi inaonyesha kwa Mungu kama Muumba: “Siku ya saba ni sabato kwa Bwana Mungu wako: ... Maana kwa siku sita Bwana akafanya mbingu na inchi, bahari na vyote vilivyo ndani yake, akapumzika siku ya saba. Kwa hivi Bwana akabariki siku ya sabato na kuitakasa.” Kutoka 20:10,11. Sabato, Bwana anasema, ni “alama, ... mujue ya kuwa mimi ni Bwana Mungu wenu.” Ezekieli 20:20. Kama Sabato ingeshikwa kwa wote, mtu angeweza kuongozwa kwa Muumba kama jambo la kuabudu. Hapo hapangalikuwa kamwe mwabudu sanamu, asiyesadiki (Mungu), wala kafiri. Kushika Sabato ni alama ya uaminifu kwa “yeye aliyefanya mbingu na dunia na bahari na chemchemi za maji.” Ujumbe unaoagiza watu kuabudu Mungu na kushika amri zake utawaita kwa kipekee muwaite kushika amri ya ine.TSHM 211.1

    Katika tofauti kuwa wale wanaoshika amri za Mungu na imani ya Yesu, malaika wa tatu anaonyesha kwa kundi lingine: “Mtu akiabudu nyama na sanamu yake, na kupokea chapa katika kipaji cha uso wake, ao katika mkono wake, yeye atakunywa mvinyo ya gazabu ya Mungu.” Ufunuo 14:9,10. Ni nini inayokuwa mfano wa nyama, sanamu, chapa?TSHM 211.2

    Unabii ambamo mifano hii inapatikana unaanza kwa Ufunuo 12. Joka yule aliyetafuta kuharibu Kristo kwa kuzaliwa kwake ilisemwa kuwa Shetani (Ufunuo 12:9); akavuta Herode kuua Mwokozi. Lakini mjumbe wa Shetani katika kufanya vita juu ya Kristo na watu wake kwa karne za kwanza ilikuwa ufalme wa Roma, ambamo upagani ulikuwa ni dini iliyoshinda. Kwa hiyo joka ni, kwa namna ya pili, mfano wa Roma ya kipagani.TSHM 211.3

    Katika Ufunuo 13 ni nyama mwingine, “mfano wa chui,” ambaye joka akamupa “nguvu zake, na kiti chake cha ufalme na mamlaka nyingi.” Mfano huu, kama vile Waprostanti wengi walivyoamini, unakuwa mfano wa dini ya Papa, iliyofuata kwa nguvu (mamlaka) na kiti cha ufalme na mamlaka iliyoshikwa kuanza na ufalme wa Roma. Juu ya nyama aliyekuwa na mfano wa chui inasemwa: “Naye akapewa kinywa cha kusema maneno makubwa, na makufuru... Akafungua kinywa chake atukane Mungu , na kutukana jina lake, na hema yake, nao wanaokaa mbinguni. Tena akapewa kufanya vita na watakatifu na kuwashinda; akapewa mamlaka juu ya kabila na lugha na taifa.” Ufunuo 13:5-7. Unabii huu, karibu kuwa sawasawa pamoja na maelezo ya pembe ndogo ya Danieli 7, unaonyesha bila shaka Kanisa la Kiroma.TSHM 211.4

    “Akapewa mamlaka kufanya kazi yake miezi makumi ine na miwili”--miaka mitatu na nusu, ao siku 1260, ya Danieli 7--mda ambao nguvu (uwezo) za Papa zilipaswa kugandamiza watu wa Mungu. Mda huu kama ilivyotajwa katika sura zilizotangulia, ulianza na mamlaka ya kanisa la Roma (Papa), A.D. 538, na kumalizika katika mwaka 1798. Kwa wakati ule mamlaka ya Papa ikapata “kidonda cha kufa,” na unabii ukatimia, “yeye anayepeleka katika kifungo atachukuliwa katika kifungo.”TSHM 212.1

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents