Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Sabato ya Kweli Kila Mara Ilishikwa

    Tangu siku ile hata sasa Sabato imeshikwa. Ingawa “mtu wa zambi” alifaulu katika kugandamiza chini ya mguu siku takatifu ya Mungu, lakini ilifichwa katika mahali pa siri roho aminifu zikaitolea heshima. Tangu wakati wa Matengenezo (Reformation), wengine katika kila kizazi wameimarisha kushikwa kwake.TSHM 220.2

    Mambo haya ya kweli katika kuhusiana pamoja na “habari njema ya milele” yatatofautisha kanisa la Kristo kwa wakati wa kutokea kwake. “Hapa ni uvumilivu wa watakatifu wanaoshika amri za Mungu, na imani ya Yesu.” Ufunuo 14:12.TSHM 220.3

    Wale waliokubali nuru juu ya Pahali patakatifu na sheria ya Mungu walijazwa na furaha kwa namna walioona umoja wa kweli. Walitamani nuru ya kugawanywa kwa Wakristo wote. Lakini kweli tafauti pamoja na ulimwengu haikukaribishwa kwa wengi waliojidai kufuata Kristo.TSHM 220.4

    Kwa namna haki ya Sabato ilivyoonyeshwa, wengi wakasema: “Tulikuwa tukishika Jumapili (siku ya kwanza) sikuzote, wazazi wetu waliishika. Kushika kwa Sabato mpya kungetutupa inje ya umoja pamoja na ulimwengu. Kundi ndogo linaloshika siku ya saba linaweza kufanya nini juu ya ulimwengu wote unaoshika Jumapili (siku ya kwanza ya juma)?” Kwa mabishano ya namna moja Wayuda wakatoa sababu zao za kukana Kristo. Vivyo hivyo wakati wa Luther, Wakristo wa dini ya Roma wakafikiri kwamba Wakristo wa kweli walikufa katika imani ya Kikatoliki; kwa sababu hiyo dini ile ilikuwa ya kutosha. Wazo la namna ile lingehakikisha kizuizi zaidi kwa maendeleo yote katika imani.TSHM 220.5

    Wengi walishurutisha kwamba kushika kwa Jumapili (siku ya kwanza ya juma) ilikuwa desturi ya kanisa iliyoenea sana ya kanisa kwa karne nyingi. Kinyume cha mabishano haya ilionyeshwa kwamba Sabato na kushikwa kwake kulikuwa kwa zamani zaidi kuliko, hata kwa zamani za ulimwengu wenyewe--uliyoimarishwa na Mzee wa Siku.TSHM 220.6

    Kwa ukosefu wa ushuhuda wa Biblia, wengi wakashurutisha: “Sababu gani watu wetu wakubwa hawafahamu swali hili la Sabato? Wachache wanaamini kama unavyo amini. Haiwezekani kuwa kwamba unakuwa na hakika na watu wote waliojifunza kuwa wakosefu.”TSHM 220.7

    Kwa kupinga mabishano ya namna hii ilikuwa tu lazima ya kuita Maandiko na matendo ya Bwana pamoja na watu wake katika vizazi vyote. Sababu mara kwa mara Mungu hakuwa akichagua watu waliojifunza na cheo kwa kuongoza katika matengenezo ni kwamba wanatumainia kanuni za imani ya kanisa na desturi za elimu ya tabia na sifa za Mungu na dini na kutoona haja kamwe ya kufundishwa na Mungu. Watu wanaokuwa na majifunzo ya chini wanaitwa nyakati zingine kutangaza kweli, si kwa sababu wanakuwa wasiojifunza, lakini kwa sababu si watu wenye majivuno ya kukataa kufundishwa na Mungu. Unyenyekevu wao na utii vinawafanya kuwa wakubwa.TSHM 221.1

    Historia ya Israeli wa zamani ni onyesho la kushangaza ya mambo ya maisha ya wakati uliopita ya jamii ya Waadventisti. Mungu aliongoza watu wake katika mwendo wakurudi kwa Yesu,ijapo kama vile alivyoongoza wana wa Israeli kutoka Misri. Kama wote waliotumika kwa umoja katika kazi munamo mwaka 1844 wangepokea ujumbe wa malaika wa tatu na kuutangaza katika uwezo wa Roho Mtakatifu, miaka iliyopita ulimwengu ungekuwa umekwisha kuonywa na Kristo angekuwa amekwisha kuja kwa ajili ya ukombozi wa watu wake.TSHM 221.2

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents