Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Kuja kwa Kristo mwenyewe

    Mafundisho juu ya kugeuka kwa ulimwengu na utawala wa Kristo wa kiroho hayakushikwa na kanisa la mitume. Kwa kawaida hayakukubaliwa na Wakristo hata karibu ya mwanzo wa karne ya kumi na mnane. Ilifundisha watu kutazamia mbali kwa wakati ujao kuja kwa Bwana na kuwakataza kwangalia ishara za kurudi kwake. Iliongoza watu kutojali kujitayarisha kwa kumlaki Bwana wao.TSHM 152.3

    Miller akaona kuja kwa Kristo halisi kulikofundishwa wazi katika Maandiko. “Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka toka mbinguni, na sauti kubwa, na sauti ya malaika mkubwa, na pamoja na baragumu ya Mungu.” “Nao wataona Mwana wa watu akija katika mawingu ya mbingu pamoja na uwezo na utukufu mkubwa.” “Kwa maana kama umeme unavyokuja toka mashariki na unaonekana hata mangaribi; ni hivi kuja kwa Mwana wa watu kutakavyokuwa.” “Mwana wa watu atakapokuja katika utukufu wake, na malaika yote pamoja naye.” “Naye atatuma malaika zake na sauti kubwa ya baragumu, nao watakusanya wachaguliwa wake.” 1 Watesalonika 4:16, 17; Matayo 24:30, 27; 25:31; 24:31.TSHM 152.4

    Kwa kuja kwake wafu wenye haki watafufuka na wenye haki waliohai watabadilika. “Sisi sote hatutalala, lakini sisi sote tutabadilika, kwa dakika moja, kwa kufunga na kufungua jicho, kwa baragumu ya mwisho: sababu baragumu italia, na wafu watafufuliwa wasiwe na kuoza, na tutabadilika. Maana sharti ule mwili wenye kuoza uvae kutokuoza, na huu wa mauti uvae kutokufa.” “Nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza; kisha sisi tulio hai, tuliobaki, tutanyanyuliwa pamoja nao katika mawingu, kukutana na Bwana katika hewa, na hivi tutakuwa pamoja na Bwana milele.” 1 Wakorinto 15:51-53; 1 Watesalonika 4:16, 17.TSHM 153.1

    Mtu katika hali ya sasa ni wa kufa, wakuoza; lakini ufalme wa Mungu utakuwa wakutokuoza. Kwa hivyo mtu kwa hali yake ya sasa hawezi kuingia katika ufalme wa Mungu. Wakati Yesu atakuja, atatoa kutokufa kwa watu wake, na kuwaita kuriti ufalme ambao hawakuuriti hata sasa.TSHM 153.2

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents