Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Katika Utetezi wa Sheria ya Mungu

    Katika kujibu madai kwamba wakati wa kifo cha Kristo, amri kumi ziliondolewa pamoja na sheria za kawaida, Wesley akasema: “Sheria ya tabia, inayokuwa katika Amri Kumi na ikatiliwa nguvu na manabii, hakuitosha. Hii ni sheria ambayo haiwezi kamwe kuvunjwa, ambayo `inasimama imara kama shuhuda mwaminifu mbinguni.’”TSHM 122.2

    Wesley akatangaza umoja kamilifu wa sheria na injili. “Kwa upande moja sheria kwa kuendelea kutuongoza kwa injili, kwa ngambo ingine injili huendelea kutuwezesha kutimiza utimilifu inafanya njia kuwa na sheria, kwa mfano, inatuamuru kumpenda Mungu, kupenda jirani wetu, kuwa wapole, wanyekevu ao watakatifu. Tukijisikia kwamba hatutoshi kwa mambo haya; ... lakini tunaona ahadi ya Mungu kutupatia upendo huo, na kutufanya wanyenyekevu, wapole, na watakatifu: tunashika injili hii, ya habari ya furaha: ... ` haki ya sheria hutimilika ndani yetu; kwa njia ya imani inayokuwa katika Yesu Kristo. ...TSHM 122.3

    “Katika daraja la juu sana za maadui wa injili ya Kristo,” akasema Wesley, “ni wale ... wanaofundisha watu kuvunja ... si moja tu, wala ndogo ao kubwa sana, bali amri zote kwa jumla. ... Wanamheshimu kama Yuda alivyofanya aliposema, `salamu, Rabi; akamubusu’ ... Hakuna namna ingine isipokuwa kumusaliti kwa kumubusu, kuzungumza juu ya damu yake, na kunyanganya taji lake; kuweka nuru kwa kila sehemu ya sheria yake, chini ya ujanja wa kuendesha injili yake.”TSHM 122.4

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents