Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Mwezi kama Damu

    “Giza ya usiku haikukosa kuwa ya ajabu na ya kutisha kama ile ya mchana; ingawa mwezi ulikuwa karibu kuwa mzima, hakuna kitu kilikuwa cha kutambulikana ila tu kwa msaada wa nuru isiyokuwa ya asili, ambayo, kama ikionekana kwa nyumba za jirani na mahali pengine kwa mbali ilionekana kama katika ile giza ya Misri ambayo ilionekana karibu kama isiyopenyeka kwa miale.” “Kama kila kitu chenye kung’aa katika ulimwengu kilifunikwa katika giza isiyopenyeka, ao kingeondolewa, giza haingalikuwa kamili kabisa.” Baada ya usiku wa manane giza ikatoweka, na mwezi, wakati ulionekana mara ya kwanza, ulikuwa na rangi ya damu.TSHM 144.6

    Tarehe 19 ya Mai 1780, inakuwa katika historia kama “Siku ya Giza.” Tangu wakati wa Musa hakuna giza ya namna ile nzito, kubwa, na yakuendelea iliyoandikwa. Maelezo yaliyotolewa kwa washuhuda waliojionea ni jibu la maneno yaliyoandikwa na Yoeli miaka 2500 mbele: “Jua litageuka kuwa giza, na mwezi kuwa damu mbele ya kutimia kwake ile siku kubwa ya Bwana yenye kuogopesha.” Yoeli 2:31.TSHM 145.1

    “Wakati maneno haya yanapoanza kuja,” akasema Kristo, “tazameni juu, munyanyue vichwa vyenu kwa sababu ukombozi wenu umekaribia.” Alitolea wafuasi wake mfano wa mti uliochipuka wakati ya mwaka ya kukua ao kuota kwa mimea: “Wakati inapochipuka, munaona na kutambua ninyi wenyewe ya kwamba mavuno yamekwisha kuwa karibu. Vile nanyi, wakati munapoona maneno haya yanapotokea jueni ya kwamba ufalme wa Mungu ni karibu.” Luka 21:28, 30, 31.TSHM 145.2

    Lakini katika kanisa upendo kwa ajili ya Kristo na imani katika kuja kwake vilipoa. Waliojidai kuwa watu wa Mungu walipofushwa kwa mafundisho ya Mwokozi juu ya ishara za kuonekana kwake. Mafundisho ya kuja kwa mara ya pili yalizarauliwa, hata ikiwa kwa, eneo kubwa, haikujaliwa na ikasahauliwa, hasa zaidi kule Amerika. Tamaa ya mali, kupigania sifa na uwezo, vikaongoza watu kuweka mbali kwa wakati ujao siku ile kubwa ambapo mambo yote ya sasa yatapaswa kupita.TSHM 145.3

    Mwokozi alitabiri hali ya kukufuru ilipashwa kuwako mbele ya kuja kwake kwa mara ya pili. Kwa wale wanaoishi kwa wakati huu, onyo la Kristo ni: “Mujiangalie, mioyo yenu isipate kulemewa na ulafi na ulevi, na masumbuko ya maisha haya, siku ile isije kwenu gafula kama mutego.” “Lakini tazameni kila wakati, mukiomba mupate nguvu ya kukimbia maneno haya yote yatakayokuwa, na kusimama mbele ya Mwana wa watu.” Luka 21:34, 36.TSHM 145.4

    Ilikuwa jambo la maana sana kwamba watu waamshwe kwa kujitayarisha kwa ajili ya mambo makubwa yanayo husiana na kufungwa kwa rehema. ‘’Siku ya Bwana ni kubwa na ya kuogopesha, nani anayeweza kuivumilia?” Nani atakayesimama wakati atakapoonekana yeye anayekuwa na “macho safi zaidi hata asiweze kutazama mabaya,” na hawezi “kutazama ukaidi”? “Nami nitaazibu ulimwengu kwa sababu ya ubaya wake, na wenye zambi kwa sababu ya uovu wao, nami nitakomesha kiburi cha wenye majivuno; nami nitaangusha chini majivuno ya wenye ukali.” “Wala feza zao wala zahabu zao hazitaweza kuwaponyesha;” “Na utajiri wao utakuwa mateka, na nyumba zao ukiwa.” Yoeli 2:11; Habakuki 1:13; Isaya 13:11; Zefania 1:18, 13.TSHM 145.5

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents