Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Biblia llifananishwa kama Habari za Uwongo

    Mitume, wanafananishwa na pepo za uwongo, wanafanywa, kwa kukanusha mambo waliyoandika wakati walipokuwa kwa dunia. Shetani anafanya ulimwengu kuamini ya kwamba Biblia ni habari za uwongo, kitabu kilichopendeza kwa utoto wa taifa, lakini, sasa kuzaniwa kama kisiuchofaa. Kitabu kinachopaswa kumuhukumu yeye na wafuasi wake anakiweka katika kivuli; Mwokozi wa ulimwengu anamfanya kuwa kama mtu yo yote. Na waaminifu katika mifano ya kiroho wanajaribu kufanya kuonekana kwamba hakuna kitu cha muujiza katika maisha ya Mwokozi wetu. Miujiza yao wenyewe, inatangaza, kwa mbali zaidi kazi za Kristo.TSHM 272.3

    Imani ya kuwa roho za watu waliokufa (spiritisme) inajitwalia sasa umbo la Kikristo. Lakini mafundisho yake hayawezi kukanushwa wala kufichwa. Katika mfano wake wa sasa unakuwa ya hatari zaidi, wa hila, udanganyifu. Inajidai sasa kukubali Kristo na Biblia. Lakini Biblia inafasiriwa kwa namna ya kupendeza kwa moyo mpya. Mapendo inakuwako kama sifa bora ya Mungu, lakini inaaibishwa kwa tamaa zaifu kufanya tofauti ndogo kati ya uzuri na ubaya. Mashitaki ya Mungu ya zambi, matakwa ya sheria yake takatifu yanachungwa mbali na kuonekana kwa macho. Mifano inaongoza watu kukataa Biblia kama msingi wa imani yao. Kristo anakaniwa kama mbele, lakini udanganyifu hautambuliwe.TSHM 272.4

    Wachache wanakuwa na wazo la haki la uwezo wa kudanganwa wa imani ya kuwa na roho za watu waliokufa (spiritisme). Wengi wanavuta vibaya nao kwa kupendeza tu uchunguzi. Wangejazwa na hofu kuu kwa wazo la kujitoa kwa utawala wa pepo. Lakini wanajitayarisha kwa kiwanja kilichokatazwa, na mharibu wautumia uwezo wake, na anawashikilia kuwa watumwa. Hakuna kitu kingine kisipokuwa uwezo wa Mungu, kwa jibu kwa maombi ya bidii, inayowezakuokoa nafsi hizi.TSHM 272.5

    Wote wanaolinda zambi inayojulikana kwa makusudi wanaalika majaribu ya Shetani. Wanajitenga wenyewe kutoka kwa Mungu na ulinzi wa malaika zake, na wanakuwa pasipo mateteo. “Na wakati wanapokuambia: Tafuta habari kwa watu wenye roho na kwa walozi wafumu, wanaolialia kama ndege na kunungunika, sema, haifai kwa watu kutafuta kwa Mungu wao? Waenda kwa watu waliokufa kwa ajili ya watu walio hai? Kwa sheria na kwa ushuhuda! Kama hawasemi sawasawa na neno hili, kweli hapana asubui kwao.” Isaya 8:19, 20.TSHM 272.6

    Kama watu wangekusudia kupokea ukweli juu ya asili ya mtu na hali ya wafu, wangeona katika imani ya kuwa roho ya watu waliokufa (spiritisme) uwezo wa Shetani na miujiza ya uwongo. Lakini wengi wanafunga macho yao kwa nuru, na Shetani anafuma mitego yake kwao. “Kwa sababu hawakupokea mapendo kwa kweli, wapate kuokolewa,” kwa sababu hii, “Mungu anawaletea nguvu ya upotevu, hata waamini uwongo.” 2 Watesalonika 2:10, 11.TSHM 273.1

    Wale wanaopinga imani ya kuwako kwa roho ya watu waliokufa (spiritisme) wanashambulia Shetani na malaika zake. Shetani hataacha hatua (=2,54cm) moja ya uwanja ila tu akisukumwa kwa nguvu na wajumbe wa mbinguni. Anaweza kutumia Maandiko na atapotosha maana ya mafundisho Wale watakaosimama kwa wakati huu wa hatari wanapashwa kufahamu wao wenyewe ushuhuda wa Maandiko.TSHM 273.2

    Pepo za mashetani wanaoiga ndugu ao rafiki watatokea kwa huruma za mapendo kwetu na watafanya miujiza. Inatupasa kuwazuia kwa njia ya kweli ya Biblia ya kwamba wafu hawajui kitu cho chote na ya kwamba wale wanaotokea ni pepo za mashetani.TSHM 273.3

    Imani yao yote haikuanzishwa kwa Neno la Mungu watadanganyiwa na kushindwa. Shetani “anatumika na madanganyo yote ya uovu, ” Na madanganyo yake yataongezeka. Lakini wale wanaotafuta maarifa ya kweli na safi nafsi zao katika utii watapata katika Mungu wa kweli ulinzi wa hakika. Mwokozi angetuma upesi kila malaika kutoka mbinguni kulinda watu wake kuliko kuacha nafsi moja inayotumaini kushindwa na Shetani. Wale wanaojifariji wenyewe kwa uhakikisho kwamba hakuna azabu kwa ajili ya mwenye zambi, wanaokataa kweli ambayo Mbingu inayotoa kama ulinzi kwa siku ya taabu, watakubali madanganyo yaliyotolewa na Shetani, madai ya imani ya madanganyo za watu waliokufa (spiritisme).TSHM 273.4

    Wenye kuzihaki wanazani mizaha matangazo ya Maandiko juu ya shauri la wokovu na malipo yatakayokuja ya wanaokataa kweli. Wanageuza jambo la kutia huruma kwa mawazo ya ushupavu, uzaifu, na mafundisho ya uchawi kama kutii matakwa ya sheria ya Mungu. Wamejitoa wote kwa mshawishi, wamejiunga karibu sana naye na kujazwa na roho yake, ili wasiwe na upungufu kutoka katika mtego wake.TSHM 273.5

    Msingi wa kazi ya Shetani uliwekwa kwa matumaini iliyotolewa kwa Hawa katika Edeni: “Hakika hamutakufa”. “Siku mutakapokula matunda yake, macho yenu yatafunguliwa, na mutakuwa kama Mungu mukijua uzuri na ubaya.” Mwanzo 3:4,5. Kipeo chake cha madanganyo kitafikia katika mabaki ya mwisho ya wakati. Asema nabii: “Nikaona pepo wachafu watatu waliofanana na vyura, wakatoka kinywa cha yule joka, na katika kinywa cha yule nabii wa uwongo kama vyura. Maana ndio pepo za mashetani, wanaofanya alama, na kutoka na kwenda kwa wafalme wa ulimwengu wote, kuwakusanya kwa vita ya siku ile kubwa ya Mungu Mwenyezi.” Ufunuo 16:13, 14.TSHM 274.1

    Ila tu wale wanaolindwa na uwezo wa Mungu katika imani katika Neno lake, ulimwengu mzima utapita kwa nguvu katika njia za madanganyo haya. Watu wanajitumbukiza upesi kwa salama ya ajali, kuamshwa tu na kumiminika kwa hasira ya Mungu.TSHM 274.2

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents