Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Ujumbe Unatawanyika

    Amerika ikawa mahali pakubwa pa kazi ya kutangaza kurudi kwa Yesu. Maandiko ya Miller na ya washiriki wake yakaenezwa duniani pote. Mbali na katika eneo kubwa habari njema ya milele: “Ogopeni Mungu, na kumutukuza kwa maana hukumu yake imekuja.”TSHM 176.4

    Mambo ya unabii ambayo ilionekana kuonyesha kuja kwa Kristo katika majira ya 1844 yakashikwa sana rohoni mwa watu. Wengi wakasadikishwa kwamba mabishano juu ya nyakati za unabii yalikuwa ya haki, na wakaacha kiburi na mafikara yao, wakakubali kweli kwa furaha. Wachungaji wengine wakaacha mishahara yao na wakajiunga katika kutangaza kuja kwa Yesu. Karibu wachungaji wachache, walakini, walikubali habari hii; kwa hivyo ikatolewa zaidi kwa watu wanyenyekevu wasiokuwa mapadri. Wakulima wakaacha mashamba yao; wafundi wa mashini, wakaacha vyombo vyao; wachuuzi wakaacha biashara yao; wafundi wa kazi wakaacha vyeo vyao. Kwa mapenzi wakavumilia kazi ngumu, taabu, na mateso, ili wapate kuita watu kwa toba kwa wokovu. Ukweli wa kurudi kwa Yesu ukakubaliwa na maelfu ya watu.TSHM 176.5

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents