Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Uhakika wa Mbinguni

    Kitu kilichotendwa katika mufano wa huduma ya Pahali patakatifu pa kidunia, inatendwa katika ukweli katika Pahali patakatifu pa mbinguni. Baada ya kupanda kwake mbinguni Mwokozi wetu akaanza kazi yake kama kuhani mkuu wetu: ” Kwa sababu Kristo hakuingia katika Pahali patakatifu palipofanywa kwa mikono, ndio mufano wa kweli, lakini aliingia mbinguni zenyewe, aonekane sasa mbele ya Mungu kwa ajili yetu.” Waebrania 9:24.TSHM 202.1

    Utumishi wa kuhani katika chumba cha kwanza, “ndani ya pazia” inayotenga Pahali patakatifu pa patakatifu kwa behewa (uwanja) ya inje, ni mufano wa kazi ambayo Kristo alianza kisha wakati alipo panda mbinguni. Kuhani katika utumishi wa kila siku akaonyesha mbele ya Mungu damu ya sadaka ya zambi, vilevile uvumba ambao unapanda pamoja na maombi ya wa Israeli. Kwa hivyo Kristo anaombea damu yake mbele ya Baba kwa ajili ya wenye zambi na anaonyesha mbele yake, pamoja na manukato ya haki yake mwenyewe, maombi ya waamini waliotubu. Hiyo ndiyo iliyokuwa huduma katika chumba cha kwanza cha Pahali patakatifu katika mbingu.TSHM 202.2

    Huko imani ya wanafunzi wa Kristo wakamfuata wakati alipokuwa akipanda. Hapa matumaini yao yalikuwa, “tumaini gani tuliyo nayo kama nanga ya roho, yote mbili kweli na kuwa imara, na inayoingia ndani ya pazia, pahali alipoingia Yesu kwa ajili yetu, mutangulizi wetu, amekuwa kuhani mkubwa kwa milele.” “Kwa damu yake mwenyewe aliingia mara moja tu katika Pahali patakatifu alikwisha kupata ukombozi wa milele kwa ajili yetu.” Waebrania 6:19,20; 9:12.TSHM 202.3

    Kwa mda wa karne ya kumi na mnane kazi hii ikaendelea katika chumba cha kwanza cha Pahali patakatifu. Damu ya Kristo ikahakikisha rehema na ukubali wa Baba kwa ajili ya waamini waliotubu, lakini zambi zao zingali zikidumu kwa vitabu vya ukumbusho. Kama katika huduma ya mfano huko kulikuwa na kazi ya upatanisho kwa mwisho wa mwaka, kwa hivyo kabla ya kazi ya Kristo kwa ajili ya watu kumalizika kunakuwa kazi ya upatanisho kwa ajili ya ondoleo la zambi kwa Pahali patakatifu. Kazi hii ilianza wakati siku 2300 zilipokwisha. Kwa wakati ule Kuhani wetu Mkubwa akaingia Pahali patakatifu pa patakatifu kwa kusafisha Pahali patakatifu.TSHM 202.4

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents