Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Ushuhuda wa Kufaa

    Mungu ametoa katika Neno lake ushuhuda wa kutosha wa kuonyesha tabia yake. Lakini akili zenye mpaka zinakuwa si zakutosha kabisa kufahamu makusudi ya Mungu. “Hukumu zake hazivumbulikani, na njia zake hazifutikani!” Waroma 11:33. Tunaweza kutambua upendo usio na mpaka na rehema iliyoungana na uwezo usio na mwisho. Baba yetu aliye mbinguni atafunua kwetu kwa namna inavyotosha kwa ajili ya uzuri wetu kujua; zaidi ya pale tunapashwa kutumainia Mkono ule unaokuwa ni Mwenye mamlaka yote, Moyo unaojaa upendo.TSHM 257.5

    Mungu hataondoa kamwe sababu zote za kutoamini. Wote wanaotafuta sababu za kuwekea mashaka yao watazipata. Na wale wanaokataa kutii hata kila kizuizi kinapokwisha kuondolewa hawatakuja kwa nuru kamwe. Moyo usiofanywa upya unakuwa katika uadui na Mungu. Lakini imani inatiwa moyo kwa Roho Mtakatifu na itasitawi kama inavyolindwa. Hakuna mtu anaweza kuwa na nguvu katika imani pasipo nguvu imara. Kama watu wakijiruhusu wenyewe kubishana, mashaka yatapata msingi zaidi.TSHM 257.6

    Lakini wale wanaokuwa na mashaka na kutotumaini hakikisho (assurance) la neema yake wanapatisha haya Kristo. Wanakuwa miti isiyozaa inayozuia nuru ya jua kwa mimea mingine, kuiletea kufifia na kufa chini ya baridi ya kivuli. Kazi ya maisha ya watu hawa itatokea kama ushuhuda usiokoma juu yao.TSHM 258.1

    Kunakuwa lakini sababu moja tu ya kufuata kwa wale ambao kwa uaminifu wanatamani kuwa huru kwa kutokuwa na mashaka. Badala ya kuuliza yale wasiyofahamu, waachwe watoe ukubali kwa nuru ambayo imekwisha kuangaza juu yao, na watapata nuru kubwa zaidi.TSHM 258.2

    Shetani anaweza kuonyesha mfano karibu sana kufanana na kweli ule unaodanganya wale wanaotaka kudanganyiwa, wanaotamani kuepuka kafara iliyohitajiwa katika kweli. Lakini ni kitu kisichowezekana kwake kushika chini ya uwezo wake nafsi moja inayotaka kwa uaminifu, kwa bei yo yote, kujua ukweli. Kristo ndiye kweli, “Nuru ya kweli inayotia nuru kila mtu anayekuja katika ulimwengu.” “Kila mtu akipenda kufanya mapenzi yake, atajua habari za yale mafundisho.” Yoane 1:9; 7:17.TSHM 258.3

    Bwana anaruhusu watu wake kupata kwa majaribu makali ya kutesa, si kwa sababu anapendezwa wala kufurahishwa katika taabu yao, bali kwa sababu jambo hili ni la lazima kwa ushindi wao wa mwisho. Hakuweza, kwa uthabiti kwa utukufu wake mwenyewe, kuwalinda kutoka kwa jaribu, kwa sababu kusudi la jaribu ni kuwatayarisha kupinga mivuto yote ya uovu. Hata waovu wala mashetani hawawezi kufunga kuwako kwa Mungu kwa watu wake kama wataungama na kuacha zambi zao na kudai ahadi zake. Kila jaribu, la wazi wala la siri, linaweza kupingwa kwa kufanikiwa. “Si kwa uwezo, wala si kwa nguvu, lakini kwa Roho yangu, Bwana wa majeshi anasema.” Zekaria 4:6.TSHM 258.4

    “Naye ni nani atakayewaumiza ninyi, kama ninyi mkiwa wenye bidii katika maneno yale yaliyo mema?” 1 Petro 3:13. Shetani anafahamu vizuri kwamba roho inayokuwa zaifu zaidi inayokaa ndani ya Kristo inakuwa na nguvu zaidi kuliko mshindani kwa majeshi ya giza. Kwa sababu hiyo anatafuta kufukuzia mbali waaskari wa msalaba kutoka kwa boma lao lenye nguvu, huku anapolala akijificha, tayari kuangamiza wote wanaosubutu kwa udongo wake. Ila tu katika kutegemea Mungu na utii kwa amri zake tunaweza kulindwa.TSHM 258.5

    Hakuna mtu anayekuwa salama kwa siku moja ao saa moja pasipo kuomba. Omba Bwana kwa ajili ya hekima kwa kufahamu Neno lake. Shetani ni mbingwa katika kutumia Maandiko, kuweka mafasirio yake mwenyewe kwa mafungu ambayo anatumaini kutuletea kikwazo. Inatupasa kujifunza kwa unyenyekevu wa moyo. Huku tunapopashwa mara kwa mara kujilinda juu ya mashauri ya Shetani, inatupasa kuomba kwa imani siku zote; “Na usitulete katika majaribu.” Matayo 6:13.TSHM 259.1

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents