Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Miller Anapata Rafiki

    “Kwa gafula,” akasema, “tabia la Mwokozi likaonekana kabisa kwa akili yangu. Inaonekana kwangu kufahamu kwamba kuna Kiumbe kizuri sana na chenye huruma kwa kufanya mwenyewe upatanisho wa makosa yetu, na kutuokoa kwa kuteseka kwa azabu ya zambi... Lakini swali likatokea, Namna gani itawezekana kuhakikisha kwamba kiumbe cha namna hii kinakuwako? Inje ya Biblia, niliona kwamba sikuweza kupata ushahidi wa kuwako kwa Mwokozi wa namna ile, ao hata hali ya wakati ujao...TSHM 151.1

    “Niliona kwamba Biblia ilionyesha tu Mwokozi wa namna ninayehitaji: na nilifazaika kuona namna gani kitabu kisichoongozwa na Mungu kilipashwa kukuza kanuni zilizolingana kabisa kabisa kwa matakwa ya ulimwengu ulioanguka. Nikalazimishwa kukubali kwamba Maandiko yanapashwa kuwa ufunuo kutoka kwa Mungu. Yakawa mapenzi yangu; na katika Yesu napata rafiki. Mwokozi akawa kwangu mkuu kuliko miongoni mwa wakuu elfu kumi; na Maandiko, ambayo mbele yalikuwa giza na kinyume, sasa yakawa taa kwa miguu yangu... Niliona Bwana Mungu kuwa Mwamba katikati ya bahari ya maisha. Biblia sasa inakuwa fundisho langu kuu, na ninaweza kusema kweli, niliitafuta kwa furaha kubwa... Nilishangaa sababu gani sikuona uzuri wake na utukufu mbele, na nikashangaa namna gani ningaliweza kuikataa... Nikapoteza onyo yote ya kusoma vitabu vingine, nikatumia moyo wangu kwa kupata hekima kutoka kwa Mungu.”TSHM 151.2

    Miller akaungama wazi wazi imani yake. Lakini rafiki zake wasiokuwa waaminifu wakaendeleya mbele na mabishano, hayo yote ambayo yalishurutisha mwenyewe kupinga Maandiko. Akafikiri kwamba kama Biblia ni ufunuo wa Mungu, Kitabu hicho kinapaswa kujieleza chenyewe. Akakusudia kujifunza Maandiko na kupata kama kila mabishano ya wazi yapate kupatanishwa.TSHM 151.3

    Akaacha maelezo yo yote, akalinganisha maandiko kwa maandiko kwa usaada wa kumbukumbu ya upande na upatanifu (concordance). Kuanzia kwa Mwanzo, kusoma shauri kwa shauri, alipoona kitu cho chote cha giza ilikuwa desturi yake kukilinganisha pamoja na maneno yote yanayoweza kuwa na uhusiano na fundisho lenyewe. Kila neno likaruhusiwa kuwa na tegemeo lake juu ya maneno yenyewe. Kwa hiyo wakati wo wote alipokutana maneno magumu kwa kufahamu alipata maelezo katika sehemu ingine ya Maandiko. Akajifunza kwa maombi ya juhudi kwa ajili ya nuru ya kiMungu maneno ya mwandishi wa zaburi: “kufunua kwa maneno yako kunaleta nuru; Kunamupa mujinga ufahamu.” Zaburi 119:130.TSHM 151.4

    Kwa usikizi mwingi akajifunza kitabu cha Danieli na Ufunuo na akaona ya kwamba mifano ya unabii inaweza kufahamika. Aliona ya kwamba mifano yote mbalimbali, mezali, vifani, kama hayakuelezwa kwa maneno yaliyotangulia haya, hupata penginepo maelezo yake kwa muunganiko wake mwenyewe ao kuelezwa kwa maandiko mengine na kufahamika kwa kweli. Kiungo kwa kiungo cha mnyororo wa kweli na kuwa ni shani ya bidii yake. Hatua kwa hatua akafuatisha mistari ya unabii. Malaika wa mbinguni walikuwa wakiongoza akili yake.TSHM 152.1

    Akatoshelewa kwamba maoni ya watu wengi ya miaka elfu (millennium) mbele ya mwisho wa dunia hayakukubaliwa na Neno la Mungu. Mafundisho haya,ya kuonyesha miaka elfu ya amani mbele ya kuja kwa Bwana, ni kinyume cha mafundisho ya Kristo na mitume wake, waliotangaza kwamba ngano na magugu yanapashwa kukuwa pamoja hata wakati wa mavuno, mwisho wa dunia, na kwamba “watu wabaya na wadanganyifu wataendelea na kuzidi kuwa waovu.” 2 Timoteo 3:13.TSHM 152.2

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents