Loading...
Larger font
Smaller font
Copy
Print
Contents

Tangu Sasa Hata Milele

 - Contents
  • Results
  • Related
  • Featured
No results found for: "".
  • Weighted Relevancy
  • Content Sequence
  • Relevancy
  • Earliest First
  • Latest First
    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents

    Kukubali Zambi

    Hatua ya kwanza kwa upatanisho na Mungu ni kukubali zambi. “Zambi ni uasi (wa sheria).” “Kwa njia ya sheria zambi inajulikana.” 1 Yoane 3:4; Waroma 3:20. Ili kuweza kuona kosa lake, mwenye zambi anapaswa kupima tabia yake kwa kioo cha Mungu kinachoonyesha ukamilifu wa tabia ya haki na kumwezesha kutambua pungufu ndani yake mwenyewe.TSHM 226.1

    Sheria inafunulia mtu zambi zake, lakini haitoi dawa. Inatangaza kwamba kifo ni sehemu ya mkosaji. Injili ya kristo peke yake inaweza kumweka huru kwa hukumu ao uchafu wa zambi. Anapashwa kuzoea kutubu mbele ya Mungu, kwa sheria yake iliyovunjwa, na imani katika Kristo, kafara ya upatanisho wake. Kwa hivyo anapata “ondoleo la zambi zile zilizopita” (Waroma 3:25) na anakuwa mwana wa Mungu.TSHM 226.2

    Je, sasa anakuwa huru kuvunja sheria ya Mungu? Asema Paulo: “Basi, tunafanyiza sheria kuwa bule kwa njia ya imani? Hapana, hata kidogo; lakini tunasimamisha sheria.” “Sisi tuliokufia zambi, namna gani tutakaa ndani yake tena?” Yoane anasema: “Kwa maana kupenda Mungu ni kushika amri zake; na amri zake si nzito.” Katika kuzaliwa kupya moyo unaletwa katika umoja pamoja na Mungu, katika upatano pamoja na sheria yake. Wakati badiliko hili linafanyika ndani ya mwenye zambi amepita toka mauti hata katika uzima, kutoka kwa kosa na uasi hata kwa utii na uaminifu. Maisha ya zamani yameisha; maisha mapya ya upatanisho, imani, na mapendo yameanza. Basi “haki ya sheria” “vita itimizwa ndani yetu, tusiotembea kufuata maneno ya mwili, lakini kufuata maneno ya Roho.” Lugha ya nafsi itakuwa: “Ee ninapenda sana sheria yako! Ni mawazo yangu muchana kutwa.” Waroma 3:31; 6:2; 1 Yoane 5:3; Waroma 8:4; Zaburi 119:97.TSHM 226.3

    Bila sheria, watu hawakubali kweli zambi yao na hawaone haja ya kutubu. Hawafahamu moyoni mahitaji yao ya damu ya upatanisho wa Kristo. Tumaini la wokovu limekubaliwa bila badiliko la asili ya moyo wala matengenezo ya maisha. Hivi mabadiliko ya kijuujuu inajaa, na makutano yanaungana na kanisa ambayo hawakuwa wenye kuungama na Kristo.TSHM 226.4

    Larger font
    Smaller font
    Copy
    Print
    Contents